HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 17, 2019

WANAFUNZI 100 WALIOFAULU VIZURI KUSOMESHWA BURE

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amepokea kiasi cha Sh. Mil. 20 kutoka kwa Balozi wa Falme za Kiarabu na wamiliki wa Erminet Khalifa AbdulRahman Al-Marzooqi wamejitolea kuwasomesha wanafunzi wa kike 100 wa shule yoyote na mkoa wowote ule ili kuchangia elimu kwa wanafunzi ambao wamefahulu vizuri kidato cha nne na kukosa ada ya kuendelea masomo.

Ambapo Mh. Makonda ameomba fedha hizo zielekezwe kwa wanafunzi wakike waliofanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne kwenye masomo ya Sayansi na kushindwa kuendelea kidato cha tano kwa kukosa ada. 

Kwa upande wake Balozi alishukuru kwa ulafiki uliokuwepo baina ya nchi yao na Tanzania na kusema uendelee Kudumu. 

"Namshukuru mkuu wa mkoa na nimpongeze kwa Maendeleo anayoendelea kufanya katika na kuwa na muungano mzuri wa nchi zetu tutaendelea kutoa ushirikiano katika maendeleo ya elimu pamoja na jamii yote nikujenga urafiki bora na imara " alisema Khalifa AbdulRahman.

"Hizi fedha zitumike kuwa somesha wanafunzi wenye hali ngumu ya maisha nasi tofauti na hapo, kila wilaya watatoa wanafunzi 20 wa kike ambao wamefanya vizuri katika mtihani wa kidato cha nne kwenye masomo ya Sanyansi ambao awana uwezo wa kupata ada ya kuendelea na masomo wapewe nafasi hizo hata kama ni mtoto wa mvuvi au Yatima au anahali ngumu ya maisha apate nafasi ya kusomeshwa popote bila kuangalia kitu chochote awe amefahuru vizuri wawe na wazazi au hanao ila anahali ngumu ya maisha"anasema Makonda. 

Aidha Makonda amemuomba Balozi huyo kutujengea uwanja wa mpira wa kimataifa utakaoingia watu kuanzia 1000 na kuendele wenye hadhi ya kimataifa.

No comments:

Post a Comment

Pages