HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 31, 2019

BILIONI 1.3 ZAKUSANYWA HALMASHAURI YA BUKOBA

Zaidi ya Sh. Bilioni 1.3  zimekusanywa na Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera kwa Mwaka  Fedha 2018/2019 ambazo ni zaidi ya asilimia 97 za mapato kwa mwaka mzima.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba,  Murshid Hashim Ngeze (pichani), katika kikao cha halmashauri hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri uliopo mkoani hapa kilicholenga  kufunga robo ya nne ya mwaka wa fedha 2018/2019.

 Ngeze amesema kuwa Halmashahuri hiyo imepiga hatua  kubwa na kudai kuwa  kuwa wakati wanaingia madarakani walikuwa wakikusanya zaidi  ya shilingi milioni mia sita kwa mwaka lakini mpaka sasa wamevuka malengo kwa 100% kwa miaka minne wakiwa kwenye uongozi.

‘’Ni jambo la kumshukuru mungu nikikumbuka tulipoanzia hadi sasa ni hatua kubwa hii ni kutokana na juhudi kubwa za Rais wetu za mapambano yenye kuleta maendeleo amesema’’
Amesema  kuwa mafanikio hayo yamekuja kutokana na kasi ya  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli katika  ya kusimamia vizuri  rasilimali mbalimbali za nchi na ndio sababu  kila kiongozi amewajibika kwa nafasi yake kuanzia ngazi ya juu mpaka ya chini kwa ajili ya maendeleo ya Watanzania wote ujumla.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni diwani wa kata ya Rukoma amesema kuwa tayari  ujenzi wa shule ya sekondari umeanza katani Rukoma ili  kutatua changamoto inayowakabili wanafunzi wa kata hiyo wanaangaika kufata huduma ya elimu umbari mrefu unaowalazimu kutembea takribani kilometa 38.

Hata hivyo Ngeze ametoa wito kwa wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja na taifa zima kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Pages