HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 14, 2019

UYUI WAPEWA MWEZI KUJIBU HOJA ZOTE ZA CAG ZILIZOSABABISHA WAPATE HATI YENYE MASHAKA

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akiwahutubia Madiwani wakati wa kikao Maalumu cha Baraza la Madiwani ya kupitia hoja ya mbalimbali  kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/18.


 
NA TIGANYA VINCENT

MENEJIMENTI ya Halmashauri ya Wilaya ya Tabora(Uyui)  imepewa Mwezi mmjoa kuhakikisha imejibu na kumaliza kujibu hoja 72 za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zilizosalia  ili ziweze kufungwa na kuondoa dosari zilizojitokeza kwenye ukaguzi uliopita. 

Hoja hizo zinahusu miradi na manunuzi mbalimbali iliyotumia zaidi ya shilingi milioni 515.4 ambayo hayana uthibitisho.

Agizo hilo na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati wa Kikao Maalumu cha Baraza la Madiwani ya kupitia hoja ya mbalimbali  kutoka Ofisi ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa mwaka 2017/18.

Alisema hoja hizo ndio zimesababisha Halmashauri hiyo kuwa kati ya Halmashauri saba nchini zilizopata Hati yenye shaka ni lazima zijibiwe kwa kuwasilisha vielelezo vitakavyothibitisha matumizi ya fedha hizo kama yalifuata taratibu.

Awali akiwasilisha taarifa Mkaguzi Mkuu wa Nje Anicet Mushumbusi alizitaja sababu zilizopelekea kupata Hati yenye shaka kuwa ni pamoja na kutokuwepo kwa uthibitisho wa fedha za Amana kiasi cha milioni 30.4, malipo yenye shaka kwa kazi hewa ya shilingi milioni 95.2.

Sababu nyingine ni manunuzi ya shajala kwa ajili ya vikao mbalimbali yenye thamani ya shilingi milioni 116.5 ambayo hayana mchanganuo na malipo yenye nyaraka pungufu kiasi cha milioni 20.4.

Mushumbusi aliongeza kuwa sababu nyingine ni pamoja na mapungufu kwa vidadisi bei zilizowasalishwa na watoa huduma kabla ya manunuzi ya vifaa vya ujenzi vyenye thamani ya milioni 200.5 na manunuzi yaliyofanyika bila ushindanishashi ya milioni 52.2.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu alisema watawachukulia hatua watumishi wote ambao wameisababishia Halmashauri hiyo kuzalisha hoja za kiukaguzi za kiukaguzi na kupata Hati yenye shaka.

Alisema watumishi ni vema wakajitahidi kuzuia hoja na zio kutoa maamuzi ambayo yanasababisha kuendelea kuzalisha hoja kila mwaka.

Katibu Tawala Mkoa wa Tabora aliitaka Menejimenti ya Halmashauri hiyo kuunda timu ya kushughulikia hoja hizo ili ndani ya Mwezi mmoja wawe wamejibu na kufutwa.
Makungu aliwaomba Madiwani kuhakikisha wanafuatia katika Kata zao ili miradi mbalimbali ya wananchi inakuwa na ubora unaotakiwa.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tabora (Uyui) Said Ntahondi alisema wameunda timu ya Madiwani na Wataalamu watakaochunguza watendaji waliosababisha wapate Hati yenye shaka ili waweze kuchukuliwa hatua.

Alisema kuwa timu hiyo inatarajia kukabidhi taarifa hiyo tarehe 22 Mwezi huu kwa ajili ya hatua nyingine.
Ntahondi alisema lengo ni kutaka kuondoa dosari zilizowasababisha wapate hati hiyo na kufanya vizuri kipindi kijacho.

No comments:

Post a Comment

Pages