HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

August 14, 2019

Dodoma Jiji FC kutest mitambo na Mbeya City

NA MWANDISHI WETU, DODOMA

TIMU ya Dodoma Jiji FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza (FDL), leo inatarajia kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Mbeya City, kwenye Uwanja wa Jamhuri jijini Dodoma.

Mchezo huo awali ulipangwa kupigwa Agosti 8 mwaka huu, lakini ilishindikana kutokana na mwingiliano wa ratiba.

Dodoma Jiji FC ambayo msimu huu imefanya usajili wa kibabe kwa nyota kutoka kwa timu za Ligi Kuu Tanzania Bara (TPL), wakiwa na lengo la kuipandisha daraja msimu ujao.

Akizungumza jijini Dodoma, Katibu Mkuu wa Dodoma FC, Fortnatus John alisema mchezo huo utakuwa mahususi kwa ajili ya kujiweka fiti na msimu mpya wa Ligi Daraja la kwanza utakaoanza Septemba 14.

Mechi hiyo itapigwa saa 10:00 jioni, Wakati kiingilio kitakua Sh. 2,000 na utakua mchezo wa kwanza wa Kocha Mbwana Makata kuiongoza timu hiyo tangu alipokabidhiwa kuchukua mikoba ya Kocha Jamhuri Kihwelo.

"Huu ni mchezo muhimu wa kujipima nguvu kama sehemu ya maandalizi ya Ligi Daraja la Kwanza ambayo sisi tutashiriki na tumenga kuhakikisha tunapanda Ligi Kuu.

" Tumeweka kiingilio cha chini ili kila Mwana-Dodoma na mpenda soka aweze kuja kuitazama Tltimu yake na kutoa hamasa kwa wachezaji wetu, tunawaomba wapenzi wa mpira wa miguu kujitokeza kwa wingi ili kuiunga mkono Timu yao ambayo sisi viongozi tunawahakikishia kuwa imesukwa upya," amesema Fortnatus.

Alisema mchezo huo pia utakua mahususi kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wapya wa kikosi hicho pamoja na benchi la ufundi kwa mashabiki wao.

No comments:

Post a Comment

Pages