HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 22, 2019

Tigo, UmojaSwitch wazindua huduma ya ATM

Kaimu Mkuu wa kitengo cha huduma za Kifedha wa Tigo Pesa, Angelica Pesha akizindua huduma ya kutoa fedha kwa njia ya ATM, pembeni yake ni Afisa Mkuu Mtendaji wa UmojaSwitch,Company Ltd, Danford Mbilinyi, uzinduzi huu umefanyika leo Dar es Salaam.

  
Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Mawasiliano ya Tigo kupitia kitengo cha Tigo Pesa imeingia ubia na taasisi ya UmojaSwitch (BCX) imezindua huduma ya kutoa fedha kwa njia ya ATM ambayo ni rahisi na ya uhakika kwa wateja wa kampuni hiyo
Ushirikiano baina ya taasisi hizo mbili ni hatua muhimu katika kuchochea agenda ya ujumuishwaji wa watu kiuchumi kwani inaifanya huduma ya Tigo Pesa kuwa zaidi ya huduma ya kifedha kwa njia ya simu na kuwa huduma ya kibenki.
Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa huduma hiyo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kifedha wa Tigo Pesa, Angelica Pesha alisema huduma hiyo mpya ni utekelezaji wa mkakati wa Tigo wa kutoa huduma za kidigitali zenye ubora ili kukidhi mahitaji ya wateja.
“Tuna furaha kuzindua huduma hii mpya ya kibenki ambayo itawapa wateja wetu uhuru wa kifedha kwa kuwa ni njia rahisi na ya haraka ya kupata pesa mahali popote kupita ATM za UmojaSwitch zilizopo maeneo mbalimbali ya nchi,” alisema Pesha.
Pesha alisema huduma hiyo mpya itarahisisha utumaji na upokeaji wa fedha kwa kutumia ATM za UmojaSwitch zaidi ya 350 zilizopo hapa nchini hivyo kuchochea ustawi wa kiuchumi kwa wateja wa Tigo.
“Ni matumaini yetu kuwa huduma hii itachochea utekelezaji wa lengo letu la kuwafikia wananchi kila kona ya nchi na zaidi kuchangia agenda ya ujumuishwaji wa watu kiuchumi.Hii inasaidiwa zaidi na mawakala zaidi ya 100,000 waliopo nchini,”alisema.
Naye, Afisa Mkuu Mtendaji wa UmojaSwitch, Danford Mbilinyi alisema ushirikiano huo utachochea ukuaji wa sekta ya fedha huku ukirahisisha upatikanaji wa huduma kwa watu wote kila mahali.
Alisema UmojaSwitch ina farijika kushirikiana na Tigo ili kuwapatia wateja uhuru wa kifedha muda wote na zaidi kuokoa muda na gharama.

No comments:

Post a Comment

Pages