HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

November 27, 2019

Mourinho aanza na rekodi Tottenham UCL

Harry Kane.
Mourinho.
LONDON, UINGEREZA

MRENO Jose Mourinho ameandika rekodi mpya katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL), baada ya usiku wa kuamkia jana kuiongoza Tottenham Hotspur ya London, Uingereza kutoka nyuma kwa mabao 2-0 na hatimaye kushinda kwa mabao 4-2.

Tottenham ilikuwa nyumbani jijini London, ambako iliibua hofu kwa mashabiki baada ya kukubali kipigo cha mabao mawili ndani ya dakika 20 kwanza kutoka kwa wageni wao Olympiacos ya Ugiriki. Mabao hayo yalifungwa na Youssef El Arabi na Ruben Semedo.

Mourinho akapata nafuu baada ya Dele Alli na Harry Kane kuisawazishia mabao hayo kunaako dakika za 45 na 50, kabla ya Serge Aurier kuipa bao la uongozi Tottenham dakika ya 73 na baadaye Kane kufunga bao la nne dakika ya 77.

Kwa mabao hayo, Mourinho ameingia katika vitabu vya kushinda kwa mara ya kwanza mechi aliyotoka nyuma kwa mabao 2-0 katika historia yake kwenye michuano ya UCL, ambayo ametwaa taji mara mbili akiwa na timu za FC Porto ya Ureno (2004) na Inter Milan ya Italia (2010).

MATOKEO LGI YA MABINGWA ULAYA JANA USIKU
KUNDI A
Galatasaray       1-1 Club Brugge
Real Madrid       2–2 PSG

KUNDI B
Crvena Zvezda    0-6 Bayern
Tottenham         4-2 Olympiacos

KUNDI C
Atalanta            2-0 Dinamo Zagreb
Man City            1-1 Shakhtar Donetsk

KUNDI D
Lok. Moscow      0-2 Leverkusen
Juventus            1-0 Atletico Madrid

Daily Mail

No comments:

Post a Comment

Pages