Mwakilishi wa Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii Bi. Imelda Kamugisha akieleza namna Serikali inavyowawezesha wananchi kuondokana na vitendo vya ukatili wakati msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili wa Kijinsia.
Msanii Shetta na G nako wakitumbuiza eneo la Mlowa Mbozi mkoani Songwe wakati msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili wa kijinsia ulipokuwa mkoani hapo.
Na Mwandishi Wetu, Songwe
Msanii Shetta na G nako wakitumbuiza eneo la Mlowa Mbozi mkoani Songwe wakati msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili wa kijinsia ulipokuwa mkoani hapo.
Na Mwandishi Wetu, Songwe
Uwepo wa kipato katika
familia hasa mwanamke akiwezeshwa kiuchumi inapunguza kuwepo kwa vitendo vya
ukatili katika jamii zetu.
Hayo yamebainishwa
Mlowa Mkoani Songwe na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Idara Kuu ya Maendeleo ya
Jamii Bi. Imelda Kamugisha wakati msafara wa kijinsia wa kutokomeza ukatili wa
kijinsia uliposimama Mkoani hapo.
Amesema kuwa Serikali
katika kupambana na vitendo vya ukatili imeanzisha mpango mkakati wa kitaifa wa
kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto uliozinduliwa mwaka 2017/2018 na
utamalizika mwaka 2021/2022.
No comments:
Post a Comment