HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 02, 2020

TANROADS TABORA YAOMBA BILIONI 23.3 MWAKA UJAO WA FEDHA ZA MATENGENEZO YA BARABARA

 Mkuu wa  Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri akifungua kikao cha Bodi ya Barabara cha Mkoa wa Tabora.
Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania(TANROAD) Mkoa wa Tabora Ndamiani Ndabalinze akitoa mada jana wakati wa ufunguzi wa kikao cha Bodi ya Barabara cha Mkoa wa Tabora.
Baadhi ya wajumbe wa kikao cha kwanza cha Bodi ya Barabara cha Mkoa wa Tabora wakifuatilia hotuba ya ufunguzi wa Kikao hicho.


Na Tiganya Vincent, Tabora

WAKALA wa Barabara Tanzania (TANROD) Mkoa wa Tabora imewasilisha mapendekezo ya shilingi bilini 23.3 kwa ajili ya matengenezo ya barabara.

Kauli hiyo imewasilishwa jana na Meneja wa Wakala wa Barbara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Tabora Ndamiani Ndabalinze wakati akitoa mada jana wakati wa kikao cha Bodi ya Barabara cha Mkoa wa Tabora.

Alisema fedha hizo zinajumuisha shilingi bilioni 21.1 toka Mfuko wa Barabara na shilingi bilioni 2.2 kutoka Mfuko wa Maendeleo.

Ndabalinze alisema kuwa kwa barabara kuu wanatarajia kutengeneza kilometa 759.9, matengenezo ya barabara za Mkoa kilometa 1,318.1 na barabara za Wilaya zenye urefu wa kilometa 2,170.3.

Alisema kupitia miradi ya maendeleo wanatarajia kukarabati kilometa 130.

Katika hatua nyingine Meneja wa TANROADS Mkoa wa Tabora Ndabalinze alisema katika kipindi cha kuanzia Septemba 2019 hadi Februari, 2020, Ofisi hiyo imepeleka maombi ya shilingi bilioni 2.4 kwa ajili ya kukarabati barabara zilizoathiriwa  na mvua.

No comments:

Post a Comment

Pages