HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 14, 2020

MVUA YASABABISHA KIFO CHA MTOTO KAGERA

 Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kagera, Hamis Dawa.

 Na Lydia Lugakila, Kagera

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoani Kagera limefanikiwa kuopoa mwili wa mtoto Mwenye umri wa mwaka mmoja  aliyefahamika kwa jina la Baraka Mwombeki  mkazi wa eneo la Nyamkazi  manispaa ya Bukoba uliokutwa umetumbukia katika dimbwi la maji lililotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Kwa mujibu wa  Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kagera, Hamis Dawa, taarifa za kuzama maji kwa mtoto huyo zimetolewa Mei 13 mwaka huu majira ya  saa moja usiku kutoka kwa askari wa zimamoto waliokuwa doria.

Askari hao wamedai kuwa wameuona mwili wa mtoto huyo katika dimbwi la maji eneo la nyamkazi katika manispaa ya bukoba, na kulazimika kwenda kuuopoa.
Dawa amesema mazingira yanaonesha mtoto huyo alitumbukia katika dimbwi wakati akicheza, huku mama mzazi wa mtoto huyo aliyetambulika kwa jina la Gisela mwombeki akishindwa kuelewa mazingira aliyopo  mtoto huyo.

No comments:

Post a Comment

Pages