HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 08, 2020

WORLD VISION YATOA VIFAA VYA KUJIKINGA NA COVID-19 VYA MILIONI 17 KWA MKOA WA TABORA

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia) akimkabidhi jana Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo mmoja ya gauni likiwa ni msaada kutoka Shirika la World Vision kwa ajili ya kutumiwa na watoa huduma wakati wa kumhudumia mgonjwa wa Covid-19.
(Picha na Tiganya Vincent).



 Na Tiganya Vincent, Tabora


SHIRIKA la World Vision Tanzania limekabidhi vifaa vya thamani ya shilingi milioni 17.1 vya kudhibiti virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wahoma kali ya mapafu ya Covid -19 kwa Mkoa wa Tabora.
 
Msaada huo umekabidhiwa leo mjini Nzega na Meneja wa Kanda wa Shirika World Vision John Masenza kwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri.

Alitaja msaada huo unajumuisha glovu boksi 990, magauni ya wahudumu wa afya ya kuwafaa wakati wa kuwahudumia wagonjwa 80 , lita 290 ya vitakasa mikono na vipasa saui kwa ajili ya utoaji wa elimu kujikinga na corona 22.

Masenza alisema msaada huo utagawanywa kwa Halmashauri zote nane za Mkoa wa Tabora ili ziwaweze watoa huduma kusaidia katika mapambano dhidi ya Covid-19.

Alisema msaada mwingine ambao ni barakoa kwa ajili ya huduma za upasuaji ziko njia na zitarajiwa kuwakabidhiwa baada ya kuwasili.

Akipokea msaada huo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mwanri alilishukuru shirika la World Vision kwa kuunga mkono juhudi za Serikali za kukabiliana na kudhibiti ugonjwa wa Covid -19.

Alisema msaada huo umekuja wakati muhimu ambapo Taifa liko katika vita ya kudhibiti ugonjwa wa Covid- 19 usiendelee kusambaa.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema wadau wote Mkoani humo wanapaswa kuungana katika vita ili hatimaye waweze kuushinda ugonjwa wa Covid-19.

Alisema msaada huo walioupokea baada ya kudhibitishwa na wataalamu wa sekta ya afya kuwa ziko vizuri zitagawanywa katika Wilaya zote za Mkoa wa Tabora kwa ajili ya kuwasaidia watoa huduma za afya ambao wanasaidia kukabiliana na ugonjwa wa Covid-19 na watu wengine ambao hajiwezi.

Mkuu huyo wa Mkoa alitoa wito kwa wadau wengine wanaoendesha shughuli zao ikiwemo za biashara na kutoa huduma mbalimbali kuendelea kushirikiana na Serikali katika mapambano dhidi ya janga la Corona.

No comments:

Post a Comment

Pages