HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 02, 2020

RC TABORA AAGIZA IGUNGA KUKUSANYA SHILINGI MILIONI 365.2 WANAZODAI

NA TIGANYA VINCENT-Tabora
 
MKUU wa Mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri, ameigiza Halmashauri ya Wilaya ya Igunga kuhakikisha  inakusanya kiasi cha shilingi milioni 365.2 ambazo inadai wadau mbalimbali katika vipindi tofauti.
Fedha hizo zinatokana na mikopo ya asilimia 10 ya vikundi na ule ilioutoa kwa Vijana Saccos ambayo hairajeshwa na fedha nyingine ambazo zilikusanywa na wakala wa kukusanya mapato ya ndani ambayo hayakuwasilishwa katika Halmashauri na kusababisha hoja za kiukaguzi.
Mwanri alitoa agizo jana wakati wa kikao maalumu cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Igunga la kupitia hoja ya mbalimbali  zilizotolewa na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2018/19.
Mkuu huyo wa Mkoa alisema kati ya hizo shilingi milioni 174.9 ni mikopo ya vikundi vya wanawake, walemavu na vijana ambayo walikopeshwa lakini hadi bado wanadaiwa.
Alisema fedha nyingine ni kiasi cha milioni 95 ambazo zilitolewa kwa Vijana Saccos katika mwaka wa fedha wa 2014/15 ambapo kati ya hizo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya wakati huo alitajwa kukopa shilingi milioni 24 na zote bado hazijareshwa.
Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kuwa fedha nyingine za Halmashauri ambazo zilizotokana na makusanyo ya mapato ya ndani ambazo bado ziko mikononi mwa Wakala ni shilingi milioni 90.2.
Alisema pamoja na Mahakama kutoa hukumu ya kuwataka kulipa fedha hizo ni kiasi kidogo kimelipwa na Mawakala hao.
Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji kuanza kukata mishahara ya walimu Wakuu wote waliokusanya kiasi cha shilingi milioni 6.1 kinyume na kiwango kilichoidhinishwa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
Alisema TAMISEMI iliagiza kila mwanafunzi achangie shilingi 1,500/- kwa ajili ya UMISETA lakini wao walichangisha shilingi 2,000/-
Mwanri alisema wahusika wote ndani ya Mwezi mmoja lazima wahusika wote watafutwe na warejeshe fedha zote za Halmashauri ya Wilaya Igunga kwa ajili ya shughuli nyingine za maendeleo.
Naye Mkaguzi kutoka Ofisi ya CAG Juma Erasto alisema katika ukaguzi wa mwaka wa fedha wa 2018/19 , Igunga imepata Hati inayoridhisha.

No comments:

Post a Comment

Pages