HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 23, 2020

Tigo yaja na Tigo Rusha mpya

NA SULEIMAN MSUYA
KAMPUNI ya mawasiliano inayoongoza kwa kutoa huduma za kidigitali nchini, Tigo Tanzania imezindua huduma mpya ya Tigo Rusha iliyoboreshwa.
Hayo yamesemwa na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Tigo Tanzania, David Umoh wakati akizungumza na waandishi wa habari kwa njia ya Zoom ambapo aliweka bayana kuwa huduma hiyo inamuwezesha mteja wa Tigo kununua muda wa maongezi pamoja na vifurushi kutoka katika maduka ya Tigo ya rejareja yanayotambuliwa na Tigo Tanzania.
“Huduma hii ya Tigo Rusha iliyoboreshwa itatolewa katika mtandao wa mauzo wa Tigo ikiwa ni pamoja na maduka ya Tigo, mawakala wa Tigo Pesa, wauzaji wa kujitegemea, pamoja na vituo vya mauzo nchi nzima. Huduma hii itaongeza wigo wa namna ya kuongeza salio kwa wateja,” alisema.
Umoh, alisema, Tigo ikiwa moja ya kampuni inayoongoza kwa huduma za kidigitali, wamejizatiti kuimarisha na kubuni njia zenye kuleta unafuu na zenye chaguzi nyingi ili kumpatia mteja fursa ya kuchagua huduma inayoendana na mahitaji yake kulingana na sehemu aliyopo na muda husika.
“Tunafanya maboresho haya ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia na maisha kwa ujumla. Wateja wetu wakae mkao wa kula kwamba sasa wataweza kununua muda wa maongezi pamoja na vifurushi kutoka kwenye maduka yetu pamoja na wauzaji wengine wanaotambuliwa na Tigo nchi nzima,” alisema.
Kaimu mkurugenzi huyo alisema Tigo Rusha haina changamoto za kuharibika kwa karatasi ya vocha za kukwangua, lakini pia huduma hii inampunguzia adha mteja kutembea na kadi za vocha pindi anapohitaji kuongeza salio kwenye simu yake.
“Tigo Rusha inawapa wateja wetu thamani ya pesa zao kwa maana huduma hii ni rahisi sana kutumia, salama na ya uhakika. Kila mteja wa Tigo atakeyenunua salio au kifurushi chochote kupitia huduma hii ya Tigo Rusha anapewa zawadi ya nyongeza,” anaeleza Umoh.
 “Napenda kuwahakikishia wasambazaji wetu wote wa vocha za kukwangua kwamba hii ni fursa mpya ya kuongeza kipato, hivyo ni fursa pia kwao kukua pamoja na Tigo na kama kampuni tutaendelea kuwaunga mkono wasambazaji wote wa vocha hizo za kukwangua kote Tanzania,” alisema Umoh.
Alisema wateja wote wa Tigo wanashauiriwa kununua muda wa maongezi pamoja na vifurushi kutoka kwa wauzaji na mawakala wa Tigo Rusha ambao wanapatikana katika maeneo yote nchini Tanzania.
Kwa upande wake Mkuu wa Masoko Tigo, William Mpinga alisema huduma hiyo ya Tigo Rusha itakuwa endelevu hivyo kuwataka watumiaji waitumie.

No comments:

Post a Comment

Pages