HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 15, 2021

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIORI IKULU CHAMWINO DODOMA

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, leo Januari 15,2021 ameongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kilichoketi Ikulu Chamwino Jijini Dodoma kwa ajili ya kupita Mapendekezo Makuu matatu.
 

Kikao hicho cha Baraza la Mawaziri kilichoketi chini ya Mwenyekiti wake Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kimepitia Mapendekezo ya Mpango wa Tatu  wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/2025/26. 

 

Aidha Kikao hicho pia kimepitia Mapendekezo ya Mwongozo wa Maandalizi ya Mpango na Bajeti  ya Serikali kwa Mwaka 2021/22 na Mapendekezo ya Mpando wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22.

No comments:

Post a Comment

Pages