HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 18, 2021

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AJUMUIKA NA WANANCHI WA ZANZIBAR KUSALIA NA KUAGA MAALIM SE


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akijumuika pamoja na Wananchi wa Zanzibar katika Sala Maalum ya Kusalia Mwili wa  aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad iliyosaliwa kwenye Viwanja vya Mnazi mmoja Wilaya ya Mjini Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja leo Febuari 18,2021.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhandisi Zena A. Said  katika Viwanja vya Mnazi mmoja Zanzibar wakati wa Ghafla ya Kusalia na kuaga Mwili wa  aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad leo Febuari 18,2021.

No comments:

Post a Comment

Pages