HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 18, 2021

TAKUKURU YAOKOA ZAIDI YA SH. MILIONI 176 ZA WALIMU WASTAAFU DODOMA

Mkuu wa Takukuru Dodoma Sosthenes Kibwengo.

Fedha zilizorejeshwa.

 

NA HAMIDA RAMADHANI, DODOMA

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma imefanikiwa kurejesha Jumla ya Shilingi Milioni 176,565,000  pamoja na nyumba moja  kwa walimu wastaafu ambao walilipishwa fedha hizo na kunyang'anywa na bwana mapesa kinyume na utaratibu.

Kutokana na hayo wito umetolewa kwa wakopeshaji wa fedha mkoani hapa kuzingatia kanuni na taratibu za nchi na kuacha tabia ya kuwatoza wananchi riba umiza.

Walimu hao wastaafu waliochukuliwa mali na fedha zao na kampuni ya GENEVA CREDIT SHOP inayomilikiwa na Abubakari Kinyuma maarufu kama Abubakari Mapesa iliyopo mjini Kondoa mkoani hapa.

Akizungumza na waandishi wa Habari leo Mkuu wa Taasisi hiyo mkoani hapa, Sosthenes Kibwengo, amesema baada ya kufanyia uchunguzi kampuni hiyo mwezi Januari 2021walibaini kuwa mmiliki wa kampuni hiyo hukopesha fedha kwa riba kubwa ambapo imepelekea wananchi kumlalamikia kutoka na mikopo umiza anayoitoa.

"Kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA wataendelea kukokota kiasi cha kodi ambacho kampuni hiyo inadaiwa huku ikiendelea kufuatilia shilingi milioni 184,586,000 za wakopeshaji 22 ambazo zinapaswa kurejeshwa na Bwana mapesa," Amesema Mkuu huyo Kibwengo.

Wakizungumza Mara baada ya kurejeshwa fedha zao wananchi hao wameishukuru taasisi hiyo kwa kuwasaidia kupata fedha zao ambazo zilichukuliwa na Bwana Mapesa kwa kuongezeka riba kubwa .

Hata hivyo wananchi wameombwa kujihadhari na mikopo umiza na kamwa wasikubali kumkabidhi kadi zao za benki au hatua za nyumba kwa mtu yeyote .

No comments:

Post a Comment

Pages