Waziri
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Machi 9, 2022 kuhusu
mafanikio ya wizara hiyo katika Mwaka Mmoja wa Rais Samia Suluhu Hassan.
Kulia ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia,
Prof. Caroline Nombo.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, akizungumza na waandishi wa habari wakati akielezea mafanikio ya Serikali ya awamu ya sita katika sekta ya elimu.
Baadhi ya wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Elimu.
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI
wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema Serikali
ya awamu ya sita imedhamiria kuboresha vyuo vya ufundi ili kuongeza wigo
wa vijana kujiajiri kwenye sekta ya ufundi.
Akizungumzia
mafanikio ya mwaka mmoja wa utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan,
Profesa Mkenda amesema dhamira hiyo imejidhihirisha kwa ujenzi wa Chuo
cha Ufundi Dodoma ulioanza Mei 28 mwaka 2021.
Amesema
hayo leo Machi 9,2022 alipozungumza na wanahabari kuhusu mafanikio ya
sekta ya elimu kwa kipindi cha mwaka mmoja wa utawala wa Rais Samia na
kumpongeza kwa uwekezaji mkubwa uliofanyika katika wizara hiyo.
“Chuo
hiki cha Dodoma kikikamilika kitakuwa na uwezo wa kudahili wanafunzi
3,000 kwa mwaka mmoja wa masomo na kuongeza fursa za elimu ya ufundi kwa
lengo la kuongeza nguvu kazi ya watu wenye ujuzi hapa nchini.
“...Tunatarajia
ujenzi wa chuo hiki utakamilika katika kipindi cha miezi 18 kwa gharama
ya Sh. bilioni 17.9 ambapo hadi Januari 2021, serikali imekwisha kutoa
Sh. bilioni 3.92 za awali. Hadi sasa ujenzi umefikia kwa asilimia 45 na
kitakamilika Desemba 30,2022,” amesema Profesa Mkenda.
Kuhusu
Vyuo vya Ufundi Stadi (VETA), Januari mwaka huu, Serikali imetoa Sh.
bilioni 30.84 kwa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (VETA) kwa ajili
ya kukamilisha ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi vya Wilaya 25 hivyo
kuongeza fursa za upatikanaji wa Elimu ya Ufundi.
Amesema
kati ya fedha hizo, Sh. bilioni 28.7 zimetolewa kupitia Mpango wa
Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya UVIKO 19 (TCRP).
Kwa
mujibu wa Profesa Mkenda, ili kuhakikisha fursa za upatikanaji wa elimu
ya ufundi inaongezeka, maeneo mengine ya mafanikio katika uimarishaji
wa Eimu hiyo ni kuendeleza ujenzi wa Vyuo vya Ufundi Stadi katika Mikoa
ambayo ilikuwa haina vyuo hivyo.
Ameitaja
mikoa hiyo kuwa ni Njombe, Rukwa, Geita na Simiyu ambapo Desemba,2021
Serikali imetenga Sh.16,830,582,822.31 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivyo
ulioanza Januari 2022.
Amesema
utoaji wa mafunzo ya Ufundi Stadi kwa Makundi Maalumu ya Vijana, ambapo
vijana 8,000 wa kitanzania watanufaika ambapo Serikali imetoa Sh.
bilioni 1.81 ili kuwawezesha kujengewa ujuzi na hivyo kujiajiri na
kuajiriwa.
*Mitaala*
Waziri
Profesa Mkenda amesema wataalam wa elimu na sekta mbalimbali wapo
kwenye mchakato wa kuboresha mtaala wa elimu ili kuondoa ukakasi uliopo
kwenye mtaala huo.
Amesema
baada ya mapitio ya sera ya elimu ya mwaka 2014 amebaini uwepo wa mambo
mazuri kwenye sera hiyo huku akishangazwa na kutotekelezwa kwa baadhi
ya mambo.
“Elimu ya
lazima ni miaka 10 lakini haikutekelezwa vitu kama hivi ni vizuri
unashindwa kujua vimekwamia wapi,” amesema Profesa Mkenda.
Amebainisha kwamba ni azma ya Rais Samia kufumua sekta ya elimu na kuona mageuzi kwenye sekta hiyo kuanzia eneo la mtaala.
“Kazi
hiyo inaendelea wataalam wamejifungia wanapitia kipengele kwa
kipengele... tutakuwa na kongamano kubwa la elimu hivi karibuni ambapo
wadau kutoka ndani na nje ya nchi watashiriki. Yatafanyika makongamano
mengine ili tupate mtaala bora wa elimu,” amesema waziri huyo.
*Elimu Maalum*
Katika
kuboresha utoaji wa elimu maalum na kuongeza nafasi za mafunzo kwa
wanafunzi wenye mahitaji maalum, Serikali inakamilisha ujenzi wa shule
jumuishi ya mfano ya Lukuledi iliyopo Masasi Mkoani Mtwara itakayokuwa
na uwezo wa kuchukua wanafunzi 620.
Serikali
imewezesha uchapaji wa vitabu vya wanafunzi wenye mahitaji maalum
katika ngazi ya Sekondari ambapo jumla ya vitabu 9,178 kwa wanafunzi 353
wasioona na vitabu 93,366 kwa ajili ya wanafunzi 3,591 wenye uoni
hafifu wa elimu ya sekondari kwa thamani ya Sh 707,000,000.
Vilevile,
Serikali imewezesha ununuzi wa vifaa saidizi kwa wanafunzi 486 wenye
mahitaji maalum wa Elimu ya Juu katika taasisi 11 za umma vyenye thamani
ya Sh. 770,000,000.
Mwaka
wa fedha 2021/22, Serikali imenunua vishikwambi (Tablets) 330 vyenye
gharama ya Sh. milioni 134 kwa ajili ya shule 15 za msingi zinazopokea
wanafunzi viziwI.
Amesema
serikali pia imenunua vitimwendo 1,334 vyenye thamani ya Sh.milioni 191
kwa ajili ya wanafunzi wenye ulemavu wa viungo waliobainika kuwa na
uhitaji katika shule za msingi na sekondari.
No comments:
Post a Comment