Kaimu Mkuu Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam Dk. Coretha Komba, akitoa hotuba yake wakati wa kufungua mafunzo ya wastaafu watarajiwa jijini Dar es Salaam leo Oktoba 26, 2022.

Baadhi ya washiriki wakimsikiliza mgeni rasmi wakati akifungua mafunzo.
Mgeni rasmi (katikati) akiwa katika picha ya pamoja.
Na Mwandishi Wetu
Chuo Kikuu Mzumbe Ndaki ya Dar es Salaam wametoa mafunzo kwa wastaafu watarajiwa ili kuwaweza kumudu maisha mara baada ya kustaafu.
Mafunzo hayo ya siku kumi yanawahusisha wastaafu watarajiwa kutoka taasisi za Umma ikiwemo Mamlaka ya Maji Arusha na Chuo Kikuu Mzumbe.
Akizungumza katika mafunzo hayo Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Ndaki ya Dar es Salaam Dk. Coretha Komba amesema ni kitu kizuri kuwandaa wastaafu ili waweze kukabilana na maisha baada ya kazi.
Chuo Kikuu Mzumbe imeandaa haya mafunzo ili watu wasichanganyikiwe mara baada ya kustaafu. Nimewasikiliza watatoa mada kutoka Chuo Kikuu Mzumbe na mada zinazowasilishwa ni nzuri sana."Alisisitiza Dkt. Komba.
Aidha
Dkt. Komba aliongeza kuwa Baada ya kustaafu tunategema tutapata kiunua
mgongo kwahiyo watu wa fedha watatuambia namna ya kutumia viinua mgongo
ili kuweza kubuni miradi ambayo itaweza kutusaidia. Pia nawapongeza kuja
kuhudhuria haya mafunzo, naamini ni mafunzo mazuri na yatawasaidia
sana.
Kwa upande wa mratibu wa mafunzo hayo Dk. Daudi Pascal Ndaki amesema sababu za kuandaa mafunzo hayo ni kuweza kuwajengea uwezo wa kuandaa mipango mikakati ya uwekezaji na matumizi ya kipato baada ya kustaafu
"Mafunzo yetu haya ni kwa ajili ya kuwaelekeza wastaafu matumizi ya mapato ili waendelee kuishi bila kufanya kazi kwa kuwekeza fedha zao” alisema Dr Ndaki.
"Mafunzo haya tumekuwa tukiyaendesha mara kwa mara. Pia tumekuwa tukiwafuatilia wastaafu ambao wamehudhuria mafunzo yetu ili kujua changamoto wanazokutana nazo baada ya kustaafu na ili kuwapatia msaada wa kitalaamu wa kutatua changamoto hizo” alisisitiza Dr Ndaki.
Akizungumza kwa niaba ya washiriki wa Mafunzo hayo Mkurugenzi wa Kitengo cha Manunuzi Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jiji la Arusha, Charles Kondela amekishukuru Chuo Kikuu Mzumbe kwa kuwapa mafunzo hayo.
"Tunaahidi kwamba tutazingatia mafunzo yote kwa vitendo na kushirikiana na Wananchi wote na sisi wenyewe kuweza kuwa mfano halisi katika jamii.











No comments:
Post a Comment