HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

March 24, 2013

MVUA YAUA DAR ES SALAAM

 Daladala likipita kwa tabu katika barabara ya Azikiwe Posta jijini Dar es Salaam leo.
 Mtaa wa Azikiwe ukiwa umefurika maji ya mvua.
 Adha ya mvua gari likiwa limetumbukia katika chemba ya maji machafu.
 Wasamaria wema wakisukuma gari la polisi lenye namba PT 0314 baada ya kuzimika barabarani kufuatia mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo ya katikati ya jijini Dar es Salaam
 Mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam leo, ilisababisha adha kubwa kwa watumiaji wa barabara, kutokana na nyingi kati ya hizo kushindwa kupitika kwa urahisi baada ya kujaa maji kama picha inavyoonesha gari lenye namba za usajili T 339 CGJ likipita kwa tabu katika barabara ya Azikiwe, katikati ya jiji.   
Wakazi wa Tabata Kisiwani wakivuka mkondo wa maji kufuatia mvua kubwa iliyonyesha katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam leo na kusababisha mafuriko. 

Habari zilizotufikiwa katika chumba chetu cha habari zinasema kuwa mvua kubwa iliyoanza majira ya saa nne asubuhi imesababisha maafa baada ya mtu mmoja kuzolea na maji ya mvua katika eneo la Tabata Reli jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Pages