Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira
Mhe. Luhaga Mpina (MB) wa Kisesa akivalishwa Scarf na Kijana Mussa Sulumbi baada ya kuwasili katika viwanja vya
makao makuu ya Jimbo vilivyopo katika mji mdogo wa Mwandoya wilayani Meatu.
Diwani wa Kata ya Lugeka (CHADEMA) Mhe. Zakayo Sarya akiongea mbela ya Hadhara haipo Pichani, akisimama pamoja na madiwani wa Jimbo la Kisesa katika mkutano wa CCM jimboni humo.
Pichani, sehemu ya Hadhara iliyokuwepo katika mkutano wa Chama Cha Mapinduzi jimboni Kisesa.
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe Luhaga Mpina (MB) wa Kisesa akihutubia wananchi wa Jimbo lake hawapo pichani katika mkutano wa kuelezea mikakati na mipango ya utekelezaji wa ilani ya CCM na utatuzi wa changamoto za jimbo la Kisesa. (Picha, Habari na Evelyn Mkokoi Afisa Habari Ofisi ya Makamu wa Rais)
Na
Evelyn Mkokoi – Mwandoya Meatu
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu
wa Rais Muungano na Mazingira ambaye Pia ni Mbunge wa jimbo la Kisesa Wilayani
Meatu, amesema waowabeza Mawaziri wa Rais Magufuli na kusema kuwa wanamuogopa
na kuwa hawawezi kumshauri wamechemsha na wanajidanganya.
Naibu Waziri Mpina (MB) ameyasema hayo leo jimboni Kisesa
alipokuwa katika Mkutano na Jimbo wenye lengo la kuelezea mikakati na mipango
ya utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na utatuzi wa Changamoto za Jimbo Hilo.
Mpina alisema kuwa Mawaziri
wa Serikali ya awamu ya tano wamekuwa wakibezwa kwa kile kinachonadaiwa
wanamuogopa Mheshimiwa Rais na hawawezi kumsogelea na kumpa ushauri.
“Naenda kinyume na kauli
hiyo kwani hao wanaosema hivyo hawaoni tunachokifanya kuzunguka usiku na mchana
kutatua kero za wananchi hii ni katika kutekeleza azma ya chama cha mapinduzi
na serikali kwa ujumla ya kuwafikia wanachi na kusikiliza na matatizo yao, juzi
nilikuwa Kahama, nikaenda Geita na Singida na leo nipo Hapa Mwandoya ningefika
vipi huko bila wananchi kuleta shida zao”. Alisisita Mpina.
“Serikali imeweza kurudisha
Hekta nyingi za ardhi zilizokuwa zikimilikiwa na watu binafsi kama Sumaye na
zitarudishwa kwa wananchi, leo mnasema vipi Mawaziri wa Magufuli hawamshauri”.
Aliuliza Mpina.
Akiendelea kuongea na wana
Kisesa Mbunge wa Jimbo Hilo Naibu waziri Mpina, aliongeza kwa kusema kuwa, Pia
Ndege aina ya Bombardier Q400
zilizonunuliwa na serikali pamoja na upanuzi wa barabara akitolea mfano wa
Barabara ya Mwenge Jijini Dar es Salaam na Barabara ya Airport ya Mwanza, vyote
vimefanyika na bado watu wanabeza bila kuona kama Mawaziri wana Mchango na
wanamsaidia Mhe. Rais Magufuli.
Akiendelea kusikiliza
changamoto za wanakisesa ikiwa ni pamoja na changamoto ya eneo la makaburi na
standi ya Mwandoya, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Meatu Bw. Mussa Isaac
Mpina alilitoea ufafanuzi na kusema kuwa jambo hilo lipo katika mpango wa fedha
wa mwaka unaokuja hivyo linasubiri utekelezaji.
Akizitaja baadhi ya
changamoto zilizotatuliwa Jimboni Kisesa ikiwa ni pamoja na Barabara, Mitandao
ya simu, upatikanaji wa maji safi na salama, na kuwepo kwa Zahanati katika mji
mdogo wa Mwandoya, Mhe Mpina alisema kuwa ndani ya muda Mfupi zahanati hiyo
itapata vifaa vya kisasa vya Ultra-Sound,
X-Ray na Fridge la kuhifadhia
Damu kwani Zahanati hiyo imeshakuwa na uwezo wa kufanya upasuaji na kutoa
huduma ya uzazi.
Akiongea kabla ya kuanza kwa
Mkutano huo Diwani wa kata ya Lugeka
CHADEMA mhe.Zakayo Sarya Maarufu kwa
jina la Trump, alisema uchaguzi uliisha wakati alipotangazwa mshindi, kazi
inayofuata ni utekelezaji wa masuala ya maendeleo bila kujali itikadi za vyama
vyetu.
“ Nawashangaa sana wapinzani
wenzangu wa wanaobeza mambo mazuri anayofanya Mhe, Rais mimi Binafsi nampongeza
sana kwa jitihada zake za kuleta maendeleo bila kubagua vyama, rangi, dini wala
kabila.
Awali akihutubia Mkutano huo
Naibu waziri Mpina aliwashuru wana Kisesa kwa kumuamini na kumuweka madarakani
tangu 2005 akiwa kijana mdogo na
kuhaidi kuwatumikia bila ubaguzi wa aina yoyote kwa manufaa ya taifa.
No comments:
Post a Comment