HABARI MSETO (HEADER)


June 27, 2014

IJUE MIKAKATI YA ASHA MUHAJI SIMBA

Na Mwandishi Wetu

MGOMBEA Ujumbe nafasi ya wanawake, Asha Muhaji (pichani), amesema kuwa, changamoto zilizopo ndani ya klabu hiyo, hasa kutokuwepo kwa umoja, mshikamano na uelewano mzuri ndiyo sabababu zilizomfanya kujitosa kuwania nafasi hiyo.

Muhaji aliyekuwa Msemaji wa klabu hiyo ya Simba, na kuonekana kufanya vema katika nafasi hiyo licha ya kuitumikia kwa kipindi kifupi anawania nafasi hiyo na wenzake wawili Jasmine Badoul na Amina Poyo, katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika kesho Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na Habari Mseto Blog, Dar es Salaam leo, Muhaji amesema, anaimani ukiwepo umoja, utafanyika usajili mzuri, na Simba itapata matokeo mazuri katika mashindano yake mbalimbali ndani na nje ya nchi.

“Simba kwa sasa hakuna umoja, na mimi nawaomba wanachama wanipe ridhaa yao, wanipe nafasi hiyo maalumu kwetu akina mama, kwani nilikuwa msemaji,japokuwa viongozi wangu walikuwa wananipa taarifa kuzisema, sasa nataka niingie na mimi nikatoe mawazo yangu uko ndani,” amesema Muhaji.

Muhaji amesema, alipokuwa Msemaji alikuwa akikutana na changamoto mbalimbali kutoka kwa watu nje, hivyo basi anaamini akiingia ndani atahakikisha anazishirikiana na wenzake ili kuzifanyia kazi changamoto hizo.

“Pia nitahakikisha kwa kusaidiana na wenzangu, tunaijenga timu bora, iwe na ushindani, na kuwa tishio Barani Afrika, pia maslai bora ya wachezaji na yapatikane kwa wakati, katiba inaudhaifu mkubwa kwani tunaifanya malekebisho tu wakati wa uchaguzi inatakiwa kufanya malekebisho, na kuitoa kwa wanachama ili wajue kabla ya mkutano mkuu,”alisema.

Amesema, atahakikisha Soka la vijana kuanzia u-15, u-17, u-20 zinakuwepo ili kupata timu nzuri kubwa ambayo itasaidia timu kubwa inakuwa bora, na kusema kuwa, yeye binafsi amekuwa akijitosa mara kwa mara kwa tiomu za vijana kwani anatambua umuhimu wao ambapo sasa atafarijika kupata ridhaa ya wanachama ili akafanye mipango hiyo.

Ameongeza kuwa, pia atahakikisha kwa kushirikiana na viongozi wenzake uwanja wao wa Bunju unajengwa ili waepuke gharama za kukodi viwanja, pia ushirikishwaji wa wanachama ndani ya uongozi, pia na kuunganisha wanawake kuwa kitu kimoja na wao waweze kujiamini na kuijenga Simba kwa sauti moja.

No comments:

Post a Comment

Pages