HABARI MSETO (HEADER)


June 27, 2014

WACHEZAJI WAMTAKA SWED NKWABI SIMBA

Na Mwandishi Wetu

WACHEZAJI wa zamani, wamesema, wao wanamuunga mkono Mgombea wa nafasi ya Makam wa Rais Swedi Nkwabi (pichani), kwa kuwa wanatambua uwezo wake, toka kipindi ajawa kiongozi ndani ya klabu hiyo mpaka sasa.

Nkwabi mgombea nafasi ya Makam wa Rais, ni mgombea mwenye nafasi kubwa ya kutwaa kiti hicho, kutokana na ilani zake alizoziandaa ili kuhakikisha Simba inasonga mbele.

Akizungumza kwa niaba ya wachezaji wa zamani, mchezaji wa zamani wa Simba Moses Mkandawile amesema, anaimani Nkwabi akitwaa nafasi hiyo, kwa kushirikiana na Rais na wajumbe wa Kamati ya Utendaji Simba itafanya vema katika kila idara.

Mkandawile aliyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam, kuwa, wamekaa kama wachezaji wa zamani na kutambua nafasi ya Makam anayefaa ni Nkwabi tu na hakuna mwingine kwa kuwa wanatambua atahakikisha Simba kunakuwepo na umoja tofauti na ilivyo sasa.

“Kwa niaba ya wachezaji wa zamani, sisi katika nafasi ya Makam wa Rais wa Simba, tunamtambua Nkwabi, kijana huyo anajua nini anakifanya, anathamini watu na kutambua uwezo na umuhimu wao, hivyo basi tunaona katika nafasi hiyo ndiye anatufaa sisi,”alisema Mkandawile.

Amesema, kuna mapungufu mengi Simba kwa sasa, mfano ubora wa kikosi, mshikamano, uthamini wa watu, suala la wadhamini na mengineyo, ambapo anaimani wanachama wakimpa kura Nkwabi atatekeleza hayo.

“Nawaomba wanachama wenzangu mje kwa wingi siku ya uchaguzi, na tumchague Makam wetu wa Rais Nkwabi kwani najua na naimani kupitia yeye na wenzake watakaoingia madarakani ataifanya Simba ipige hatua zaidi ya hivi sasa, tunamuamini, tunamjua anaweza mpeni kura zenu,”alisema Mkandawile.

Mkandawile aliongozana na wachezaji wengine mbalimbali wa zamani akiwemo Idd Seleman, Fikiri Mgoso, Sunday Juma, Mlota Soma, Athumain Idd na wengine wengi ambao walifuatana naye kumuunga mkono Nkwabi.

No comments:

Post a Comment

Pages