HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 07, 2014

CHADEMA KWENDA MAHAKAMANI KUSIMAMISHA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA TEMEKE

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), leo kinatarajia kwenda Mahakamani kusimamisha uchaguzi wa Serikali za mitaa wilayani Temeke kutokana na kuenguliwa mgombea wake wa nafasi ya uenyekiti katika mtaa wa Kurasini Mjimpya.

Hayo yalisemwa jijini Dara es salaam na mgombea wa chama hicho, Thomas Odera wakati alipokuwa akitoa malalamiko yake kuhusu hujuma zinazofanywa na wasimamizi wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Desemba 14 mwaka huu.

Alisema, chama hicho kitafanya hivyo kwasababu madai yaliyotolewa na mpizani wake kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwalimu Milongea, kuwa siyo raia hayana msingi.
Alisema baada madai hayo, alitakiwa apeleke nyaraka zote zinazothibitisha uraia wake katika Kamati ya Rufaa ya Wilaya ya Temeke, ambapo Novemba 27 alifanya hivyo.

“Nilipeleka vyeti vyangu vyote vya shule ya sekondari, Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), ikiwemo cha kuzaliwa, hata hivyo, nashangaa Mlongea kusema kuwa mimi siyo raia wakati mwaka 2006 aliwahi kuwa msimamizi wangu niliponunua kiwanja.

“Unajua baada ya kuenguliwa Novemba 27 mwaka huu nilikata rufaa kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa ya Wilaya ya Temeke, Lawrence Malagwa ambako nako ilishindikana,”alisema Odero.
Odero, alisema kuwa Novemba 28 mwaka huu alipokea barua kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya rufaa ya Wilaya, Malagwa.

Katika barua hiyo, Malagwa, alisema kuwa nyaraka alizowasilisha kwa Msimamizi wa Uchaguzi hazikujitosheleza kuthibitisha uraia wake hivyo basi uwamuzi wa kuenguliwa unabaki kama ulivyo.
Odero, alisema kutokana mazingira hayo Chadema inaamini haki ya mgombea wao itapatikana mahakamani hivyo ndio maana kimeamua kuchukua hatua hiyo kikatiba.

No comments:

Post a Comment

Pages