HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 28, 2016

REKODI YA SERENGETI YAIVUTIA KENYA

Mratibu wa timu ta Tanzania kutoka Shirikisho la Soka la Kenya, Anthony Achia, amesema walikuwa wanafuatilia michuano hiyo na mafanikio ya Serengeti. “Timu imefanya vema, ikitunza hii inaweza kuitoa Afrika Mashariki kimasomaso. Unajua sisi sote ni wa East Africa (wa Afrika Mashariki). Sasa ukiona mwezako anafanya vema, lazima useme. Endeleeni. Itakuja kuirithi hii”
Katika mashindano ya AIFF, timu hiyo pekee kutoka Afrika na ambayo ilikua kipenzi cha mashabiki katika jiji la Goha ilicheza na timu ambazo ziko juu katika hatua za juu katika mtoano wa kuwania kushiriki Kombe la Dunia kupitia mabara yao yaani CONCACAF (USA) na AFC (India, Korea na Malaysia). Haishangazi nchi nyingi za Ulaya, Asia na Marekani zimeulizia uwezekano wa timu hii kutembelea nchi zao kwa michezo ya kirafiki.
Awali timu ya Serengeti Boys ilipewa nafasi ndogo ya kufanya vizuri kwa sababu ya rekodi zilizokuwa zinaiweka Tanzania katika viwango vya chini katika umri huo kwa nchi za Afrika Magharibi na Kaskazini zilikuwa juu zaidi na vilevile ukweli wa kwamba timu kama USA, Korea, Malasyia na India zilikuwa na bajeti kubwa iliyogharamiwa na Serikali zao na walikuwa na vifaa vya kila namna kiasi cha kuomba magari kwa ajili ya vifaa vya mazoezi na mechi.
Kikosi cha Serengeti kinavunja kambi kabla ya kurejea siku si nyingi ili kujiandaa na mchezo wa kufuzu fainali za Afrika chini ya miaka 17 (Madagascar 2017) dhidi ya Ushelisheli hapa tarehe 25 Juni katika uwanja wa Taifa Dar es salaam.
Benchi la ufundi limeahidi kuendelea kukiimarisha kikosi hiki na vilevile kutengeneza mpango endelevu wa kuwa na wachezaji bora zaidi kila mwaka.

Serengeti Boys ilimaliza Mashindano ya AIFF katika nafasi ya tatu kwa kuifunga Malaysia mabao 3-0.

Serengeti Boys na Bingwa Korea hawakupoteza mchezo hata mmoja na awali walipokutana walitoka sare ya 2-2.

No comments:

Post a Comment

Pages