HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 09, 2013

LIONEL MESSI: SASA NATAKA UBINGWA WA KOMBE LA DUNIA

BARCELONA, Hispania

“Kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia ndicho kitu kinachokosekana. Ni ukweli, ndiyo, ningependa kubadilisha tuzo ya ‘Ballon D’Or’ kwa Kombe la Dunia, Nimekuwa daima nikihisi hivyo. Hakuna cha kufananisha na kutwaa ubingwa wac dunia”

SAA 24 tangu alipoptangazwa kushinda tuzo ya nne mfululizo ya Mwanasoka Bora wa Dunia ‘Ballon D’Or,’ mshambuliaji Lionel Messi amedai kuwa kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia ndio kitu pekee kinachokosekana katika soka lake kwa sasa.

Messi nyota wa FC Barcelona na timu ya taifa ya Argentina, alifanmikiwa kutwaa tuzo hiyo juzi jijini Zurich, Uswisi, akiwapiku Andres Iniesta na Cristiano Ronaldo aliokuwa akichuana nao.

Mkali huyo mwenye miaka 25, amekiri kuumia kushindwa kuwika kwake na kuiwezesha Argentina kutwaa Kombe la Dunia, ubingwa ambao utamuweka yeye daraja moja na wakali kama kina Diego Maradona na Edson Arrantes de Nescimento ‘Pele.’

Messi alisema: “Kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia ndicho kitu kinachokosekana. Ni ukweli, ndiyo, ningependa kubalisha tuzo ya ‘Ballon D’Or’ kwa Kombe la Dunia, Nimekuwa daima nikihisi hivyo. Hakuna cha kufananisha na kutwaa ubingwa wac dunia.

“Nataka kupata mafanikio mengi nikiwa Barcelona na pia kwa timu yangu ya taifa ya Argentina, ambayo daima nimekuwa nikisema ndio ndoto yangu kuu niliyonayo.”

Jaribio la awali la Messi kutimiza ndoto ya kutwaa ubingwa wa Dunia litakuwa katika fainali zijazo hapo mwakani, atakapokuwa akijaribu kutwaa ubingwa katika ardhi ya mahasimu wao na wenyeji wa fainali hizo Brazil.

Ingawa alishinda ubingwa wa Kombe la Mfalme ‘Copa Del Rey’ tu akiwa na Barca msimu uliopita, Messi aliwafunika wakali wenzake na kumpa tuzo ya nne mfululizo kutokana na mabao 91 aliyofunga kwa kalenda ya mwaka 2012.

Mshambuliaji wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo alishika nafasi ya pili katika kinyang’aro ambacho nyota mwenzake na Messi, Andres Iniesta, ambaye alitwaa ubingwa wa Euro 2012 akiwa na Hispania, alishika nafasi ya tatu.

Messi aliweka rekodi ya kufunga mabao 50 katika mechi za Ligi Kuu ‘La Liga’, lakini pia akiweka rekodi nyingine ya kuwa mchezaji wa kwanza kufunga mabao matano katika mechi moja ya Ligi ya Mabingwa, ambayo Barca ilishinda 7-1 dhidi ya Bayer Leverkusen.

No comments:

Post a Comment

Pages