MKUU wa Kitengo cha ICT kutoka Benki ya Diamond Trust Tanzania, Stella
Mosha (kushoto) akitoa zawadi kwa mmoja wa washindi wa kampeni yao ya
'miaka 70 jiunge nasi ushinde',Said Mpanju kutoka Kibaha Mkoani
Pwani, mwishoni mwa wiki. (Na Mpiga Picha Wetu)
Na Imma Matukio Blog
BENKI ya Diamond Trust Tanzania (DTBT) imeanzisha kampeni maalum kupitia mitandao ya kijamii ambayo inalenga kutoa uelewa juu ya huduma wanazotoa kwa wateja na wadau mbalimbali. Mbali na hayo kampeni hiyo iliyopewa jina la 'miaka 70 jiunge nasi ushinde' imedhamiria kuwapa wadau wake zawadi mbalimbali hususani wanaowafuatilia kupitia mitandao ya kijamii ukiwemo Facebook.
Hayo yalibainishwa Jana kupitia taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na benki hiyo huku ikisisitiza zawadi nyingi zitaenda kwa watakaokuwa wanajibu vema maswali kupitia mitandao hiyo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo maswali mengi yatakuwa katika ukurasa wa benki wa,www.Facebook.com/DTB Tanzania.
No comments:
Post a Comment