HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 09, 2016

WANAFUNZI WA SHULE YA MSINGI CHANIKA WILAYANI HANDENI WAMTUMA MKUU WA WILAYA KUFIKISHA SALAMU ZAO KWA RAIS MAGUFULI

go1
Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe akifurahia wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya kuzungumza nao jambo alikutana nao waliokuwa walipomaliza kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni mkoani Tanga.

Wanafunzi hao wamemwambia Mkuu wa wilaya Mh. Godwin Gondwe kufikisha salamu zao kwa Rais Dk. John Pombe Magufuli, wakimshukuru kwa kuwezesha elimu ya Msingi mpaka Sekondari kuwa bure , kwani itarahisha wanafunzi wengi ambao wazazi wao hawana uwezo kupata elimu. Wameongeza kuwa "Mtihani ulikuwa mzuri hivyo watafauru kwa kishindo".
go02
Mkuu wa wilaya ya Handeni Mh. Godwin Gondwe Akipiga picha ya pamoja na wanafunzi wa darasa la saba mara baada ya wanafunzi hao kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi katika shule ya Chanika wilayani Handeni.
go2
Wanafunzi wa shule ya Msingi Chanika wilayani Handeni wakifurahia jambo mara baada ya kumaliza elimu ya Msingi.

No comments:

Post a Comment

Pages