HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

October 28, 2016

KUMBUKUMBU

OMUTWALE Paschal Rutaihwa Kakiziba

13 JULAI 1935 – 28 OKTOBA 2004


Baba yetu mpendwa umetimiza mwaka wa 12 tangu ulipotwaliwa na Bwana. Picha yako inatukumbusha uwepo wako tulipokuwa sote hapa duniani, na hasa ukarimu, upendo, upole, uchangamfu na wingi wa busara.

Ni vigumu kukubali kwamba haupo nasi lakini hatuna budi kuamini kwamba uko nasi kiroho kwa vile tunaye Mungu ambaye anaendelea kututia nguvu kila iitwapo leo. Busara zako na ucheshi wako vinazidi kutuimarisha kila siku na tunaendelea kuzingatia maneno yako uliyokuwa ukihimiza juu ya kuwa na upendo na umoja katika familia huku tukiendelea kumtumaini Mungu wetu ambaye amekuita kwake.

Mke wako Mary-Hilda Kakiziba, rafiki yako Galita, watoto wako, wajukuu, wakwe zako, dada zako, kaka zako na wadogo zako, ndugu, marafiki na majirani wanakosa ucheshi na ushauri wako na wanakukumbuka daima.

MISA YA KUMBUKUMBU ITAFANYIKA JUMAPILI, OKTOBA 30, 2016, SAA 3 ASUBUHI KWENYE KIGANGO CHA MT. ANTHONY WA PADUA, BOKO, DSM.

Tumaini letu linajengwa na neno lisemalo: ”Umevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo umeumaliza na imani umeilinda” (2Tim. 4:7)

Tunakuomba Ee Bwana uendelee kuipumzisha roho yake

mahali pema peponi, AMEN.

No comments:

Post a Comment

Pages