HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 06, 2017

Bank M roho kwatu kuzidi kupata faida


NA  MWANDISHI WETU
BENKI M Tanzania, imefunga mwaka wa fedha wa 2016 kwa kasi ya aina yake kwa kupata ongezeko kubwa la rasilimali zake kufikia  kiasi  cha trilioni 1 mwishoni mwa mwaka 2016.

Kwa mujibu wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Benki hiyo, Bi. Jacqueline Woiso, ni moja ya  mafanikio makubwa kwa benki hiyo.

“Mafanikio ya Benki kwa mwaka 2016, yamekuwa mazuri sana. Kwa ujumla, yanatupa  matumaini makubwa na tunavyouanza  mwaka huu mpya, tukiamini utakuwa wa mafanikio makubwa,”  alisema.

Kuhusu rasimali  za Benki, Bi. Woiso alisema zimeongezeka kutoka bilioni 977.66 kwa mwaka 2015 hadi 1,051.89 bil mwishoni mwa mwaka 2016.

Alisema mapato ya benki  yametokana na kuongezeka kwa mikopo iliyotolewa  kwa wateja  ambayo imeongezeka  kufikia  sh 806 bil kwa Desemba  2016 toka shilingi 754.78 bil iliyofikiwa  katika mwaka 2015.

Bi. Woiso alisema faida kabla ya kodi  imeongezeka kwa asilimia 35 kutoka sh 17.49 bilioni mwaka 2015 hadi sh 23.66 bilioni mwaka 2016.

Alisema sehemu kubwa ya faida  imetokana na mapato yatokanayo na riba  ambayo yameongezeka kufikia  sh 94.63 bilioni ikiwa ni ongezeko la asilimia 30.09, ikilinganishwa na mwaka 2015.
 Kuhusu amana, alisema zimeongezeka kwa asilimia 2% kufikia bilioni 805.94, mwishoni mwa mwaka 2016.

Alisema, benki hiyo imezidi kutoa  huduma bora zaidi kwa wateja wake kwa mwaka huu, huku wakiendelea kuimarisha zaidi timu yao wafanyakazi ambao wamekuwa siri ya mafanikio hayo.

Katika hatua nyingine, Benki hiyo ipo katika mikkati ya kuzidi kuboresha  mfumo uliopo wa teknolojia  ya kibenki, mfumo unaojulikana kama  Flexcube 12 kutoka kampuni ya  Oracle Financial  Service.

Kwa upande wa bidhaa, Bank M ilizindua bidhaa mpya katika soko inayoitwa Money inayowzesha wateja kupaki hundi kwa ajili ya malipo moja kwa moja  kutoka  ofisi zao bila  kutumia njia za kizamani ya mteja kutembelea matawi ya kibenki kuweka.
Bi. Woiso alisema kwa mafanikio hayo, mwaka 2016 ilipata tuzo ya Benki bora  katika sekta ya biashara za makampuni Tanzania.
Mkurugenzi Mkuu wa Bank M, Jacqueline Woiso akitoa taarifa ya ripoti ya fedha ya mwisho wa mwaka 2016 jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Fedha, Yahaya Mbanka. (Picha na Francis Dande).

No comments:

Post a Comment

Pages