HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 26, 2018

Haloteli yaboresha mfumo wa mauzo na usajili ya laini

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Halotel, Mhina Semwenda, akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu uboreshwaji wa mfumo wa uuzaji na usajili wa laini za simu. Kushoti ni Meneja Uhusisno wa  Halotel Stella Pius. (Na Mpiga Picha Wetu).

Na Mwandishi Wetu 
 
Kampuni ya mawasiliano ya simu ya Halotel, imetangaza kuboresha mfumo wake wa mauzo na usajili wa laini za simu na sasa watakaofanya hivyo ni mawakala waliothibitishwa.
Uamuzi huo ni mkakati wa kudhibiti usajili na mauzo ya laini za simu za Halotel ikiwa ni hatua ya kukabiliana na udukuzi au udanganyifu wowote unaoenda kinyume na sheria za mawasiliano nchini.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Mkuu wa kitengo cha mawasiliano wa Halotel,  Mhina Semwenda, amesema kampuni hiyo imepunguza idadi ya mauzo ya laini za simu kwa mawakala, lakini pia mawakala watauziwa laini nyingine mpya mara tu watakapokuwa wamemaliza mauzo ya laini za simu za awali pamoja na kuthibitisha kuwa laini walizopewa zimesajiliwa kwa wateja kwa kufuata taratibu zote za usajili zilizowekwa na mamlaka husika”.
“Tumeweka mfumo thabiti wa kudhibiti uuzaji wa laini za simu na usajili kutoka kwa mawakala wetu, hili pia limeambatana na uhakiki na usajili mpya wa mawakala wote wanauoza laini za simu za Halotel. Alisema Mhina na Kuongeza,
“Tumewekeza kwenye teknolojia ya kisasa zaidi itakayogundua na kuzuia udukuzi wa aina yoyote ya mifumo ya mawasiliano, Tunafanya haya yote ili kuongeza ufanisi pamoja na kuwadhibiti watu wenye nia ovu ya kutumia miundombinu ya mawasiliano kuvunja sheria” alisema Semwenda.
Alisisitiza kuwa mara zote, kampuni hiyo inafuata kanuni na sheria zilizopo ndiyo maana imekuwa ikiwekeza fedha nyingi ili kufikisha huduma bora kwa Watanzania hivyo haipo tayari kushuhudia watu wenye niaovu  wakiharibu malengo mema yaliyopo.
“Uwekezaji mkubwa uliofanywa kwa miaka miwili iliyopita nimatokeo ya ushirikiano mwema baina ta Tanzania na Vietnam. Ni uhusiano huo uliochangia kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi hizi mbili hivyo Halotel itaendelea kuzingatia sheria na kanuni za nchi pamoja na kuendelea kuboresha na kutoa huduma zenye gharama nafuu kwa Watanzania,” alisema Semwenda.

No comments:

Post a Comment

Pages