HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 12, 2018

NMB yatwaa Tuzo ya Euromoney mwaka sita mfululizo

  Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NMB, Ineke Bussemaker, akipokea Tuzo ya Benki Bora Tanzania 2018, kutoka Jarida la Euromoney la nchini Uingereza. Tuzo hiyo ni ya mwaka wa sita mfululizo kwa NMB kushinda miongoni mwa mabeki ya Tanzania. (Na Mpiga Picha Wetu).

 NA MWANDISHI WETU

JARIDA kongwe nchini Uingereza linalojihusisha na masuala ya utafiti wa kiuchumi na kibiashara la Euromoney, limeitangaza Benki ya NMB, kuwa Benki Bora ya Mwaka nchini Tanzania, ikiwa ni mwaka wa sita mfululizo. 

Tuzo hiyo iliyotolewa juzi jijini London, inaifanya NMB kuwa Benki Yenye Faida Zaidi Tanzania, inatokana na uimara wa taasisi hiyo katika Sekta ya Fedha, ilikofanya vema kupitia mabadiliko ya kimfumo yanayohusisha huduma za kidijitali.

Ikizungumzia mafanikio hayo, Euromoney katika taarifa yae limesema NMB kuwa Benki Bora Tanzania, kumezingatiwa vitu vingi, ikiwemo utoaji elimu za kifedha, mabadiliko ya kimfumo katika fedha na kutanua fursa za jamii kutumia huduma za kifedha.

Taarifa hiyo iliongeza kuwa uwekezaji wa NMB katika teknolojia, umeleta ufumbuzi wa changamoto za kushughulikia mahitaji ya wateja kwa njia za kimtandao (mobile banking), kadi za benki na mawakala wanaotoa huduma. 

Akizungumzia mafanikio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa NMB, Ineke Bussemaker, amesema benki yake inajisikia fahari na kujivunia ushindi wa khistoria waliouweka kwa kuibuka washindi wa tuzo hiyo kwa miaka sita mfululizo.

Alibainisha ya kwamba, wanapenda kutumia fursa hiyo kuwashukuru wateja wao, ambao ndio wanaowasukuma katika kuwabunia huduma bora na kwamba wanaichukua tuzo hiyo kama chachu ya kuendelea kutanua huduma bora kwa jamii.

Bussemaker alisisitiza kuwa, benki yake inajivunia uanzilishi wa mabadiliko ya kimfumo kwenda dijitali, ambayo ni sehemu ya mchakato wao wa huduma bora kwa wateja na kwamba tuzo hiyo ni matunda ya safari ya ushirikiano baina ya benki na wateja wao.

No comments:

Post a Comment

Pages