HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 04, 2018

WAHITIMU CHUO KIKUU MZUMBE WATUMIA UJUZI WALIOUPATA KUBUNI BIDHAA ZA AINA TOFAUTI

 Mkuu wa Mawasiliano Chuo Kikuu cha Mzumbe Bi. Sylivia Lupembe akimtambulisha Sia Nshiu mhitimu wa Programu ya Intrepreneuship "Trade Promotion For Industrial Development" katika  Chuo hicho ambaye yupo katika maonyesho  ya biashara ya Sabasaba kwenye viwanja vya TANTRADE barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam leo  akionyesha bidhaa zake za kahawa na mvinyo huku Waziri wa viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijage akimsikiliza wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara  RANTRADE  Bw. Edwin Rutageruka.
 Sia Nshiu mhitimu wa Programu ya Intrepreneuship "Trade Promotion For Industrial Development" katika  Chuo Kiku cha Mzumbe akitoa maelezo ya bidhaa zake kwa  Waziri wa viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijage wakati alipotembelea banda la chuo hicho katika maonyesho ya Sabasaba Barabara ya Kilwa jijini Dar es salaam kulia ni Mkuu wa Mawasiliano Chuo Kikuu cha Mzumbe na wa pili kutoka ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara  RANTRADE  Bw. Edwin Rutageruka.
 Waziri wa viwanda na Biashara Mh. Charles Mwijageakifurahia jambo na Mkuu wa Mawasiliano wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Bi. Sylivia Lupembe wakati alipomaliza kutembelea katika banda hilo kushoto ni Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara  RANTRADE  Bw. Edwin Rutageruka.
 Bw Innocent Mgeta Afisa Udahili Mwandamizi akiwapa maelezo baadhi ya wananchi waliofika katika banda hilo.Bw Innocent Mgeta Afisa Udahili Mwandamizi akiwapa maelezo baadhi ya wananchi waliofika katika banda hilo.
Bi Sia Nshiu akitoa maelezo kwa Bi Masha Kimaku aliyetembelea katika banda hilo.
...............................................................................
Na Said Mwishehe, Globu ya Jamii
WAHITIMU wa Chuo Kikuu cha Mzumbe  mkoani Morogoro wameamua kutumia taaluma ambayo wameipata chuoni hapo kufanya shughuli za ujasirimali kwa kubuni bidhaa za kipekee.
Baadhi za wahitimu hao ambao wamepikwa vema na Chuo Kikuu cha Mzumbe wameonesha kwa vitendo kuwa elimu ambayo wanaipata chuoni hapo ni mkombozi kwa Watanzania huku wakijivunia bidhaa ambazo wanazalisha kwa ubora wa hali ya juu.
Mmoja wa wahitimu wa Chuo kikuu cha Mzumbe Sia Mshiu akiwa kwenye Banda la Chuo hicho katika Maonesho ya biashara ya kimataifa yanayoendelea viwanja vya Sabasaba jijini Dar es salaam amesema kuwa kutokana na elimu ambayo ameipata ameweza kuzalisha Wine na Kahawa.
“Elimu ambayo nimeipata darasani imenifanya sasa niwe mjasiriamali na nimeweza kubuni bidhaa zangu ambapo kwa sasa natengeneza Kahawa na Wine.
“Kahawa ambayo naitengeneza ina ladha ya aina yake ambapo pia wakati wa kuitengeneza nachanganya na viungo na hivyo kuwa na aina Fulani ya ladha ambayo huwezi kuipata kokote zaidi ya kahawa ambayo natengeneza,”amesema Mshiu.
Amefafanua kutokana na kufanikiwa kutengeneza bidhaa hizo lengo lake ni kuhakikisha anasajili Mamkala ya Chakula na Dawa(TFDA)na baadae Shirika la Viwango Tanzania(TBS) ili kuifanya iwe rasmi na kuingiza sokoni.
Ametoa ombi kwa Rais Dk.John Magufuli kuwa iwapo itawezekana anatamani kuona kunaandaliwa mazingira mazuri ambayo yatajenga daraja la kuunganisha wajasiriamali wadogo kama yeye na kisha kuwaunganisha na wawekezaji wakubwa ili kuhakikisha siku moja nchi yetu inapiga hatua ya kimaendeleo.
Chuo kikuu cha Mzumbe kimeweka utaratibu wa kuhakikisha wanafunzi ambao wamemaliza kwenye chuo hicho kuendelea kuwafuatilia na kuwaendeleza katika shughuli ambazo wanazifanya.

No comments:

Post a Comment

Pages