HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

July 15, 2018

WATANZANIA WANG’ARA MAJIMAJI SELEBUKA MARATHON

 Kamanda Camillius Wambura (kushoto), akiwa na Abdurhaman Hamis wakishiriki Majimaji Selebuka Festival mjini Songea.
Wanariadha Mohamed Dulle na Geofrey Korosi wakichuana katika mbio za Kilomita 21 Majimaji Selebuka Marathon mjini Songea.

NA MWANDISHI WETU
TAMASHA la Majimaji Selebuka 2018 limekata utepe jana mjini hapa kwa mbio za Marathon huku ikishuhudiwa Nestory Hudu kutoka Singida akiwatoa nishai Wakenya.
Hudu aliibuka kidedea katika mbio za Kilomita 42 kwa Wanaume akitumia saa 2:21:25 akifuatiwa na John Leonard wa Arusha saa 2.22:09 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Simon Lelei kutoka Kenya saa 2.22:54.
Kwa upande wa Wanawake Kilomita 42 mshindi aliibuka Purity Biwott wa Kenya alishinda akitumia saa 2.43:59 akifuatiwa na  Dorcus Chesang pia wa Kenya aliyetumia saa 2.45:21 huku nafasi ya tatu ikienda kwa  Angel John wa Arusha aliyetumia saa 2:53.44.
Kwa upande wa Kilomita 21 Wanaume  Pascal Sarwat wa Manyara alishinda akitumia saa 1.11:58 akifuatiwa na  Samson Lyimo wa Songea saa 1.12:13 huku Mohamed Dulle wa JWTZ Ruvuma akikamata nafasi ya tatu akitumia saa 1:12:34 wakati kwa Wanawake Tabitha Kibeth wa Kenya alishinda akitumia saa 1.21: 34 kutoka Kenya akifuatiwa na Violeth Adam wa Njombe akitumia 1.22:43 huku nafasi ya tatu ikikosa mshindi
Kwa upande wa Walemavu Kilomita 21 mshindi aliibukaDavid Mabula akifuatiwa na John Stephano huku nafasi ya tatu ikinyakuliwa na Mathias Jollo wote kutoka Dar es Salaam.
Pia kulikuwa na Mbio za Mita 800 kwa wanafunzi ambao walitia for a kwa mwitikio mkubwa na vipaji, kwa wavulana Felix Ndunguru alishinda akitumia dakika 2.46:00 akifuatiwa na Bashiru Ngonyani dakika 2:49.2 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Franco Justine aliyetumia dakika 2:52.
Kwa wasichana Magreth Thadei alitumia 2:58.53 akifuatiwa na Hadija Mohamed dakika 2:58.55 huku nafasi ya tatu ikienda kwa Maisha Mwera dakika 2:59.03.
Mbali na washindi kujizolea zawadi ya fedha taslimu na medali, pia walipata ofa ya kutembelea Mbamba Bay Beach.
Majimaji Selebuka Festival imeandaliwa na Taasisi isiyo ya kiserikali ya Songea-Mississippi (SO-MI), kwa kushirikiana na Tanzania Mwandi chini ya udhamini wa Bakhresa Group of Companies, Premier Bet, BIT Tech Ltd/Meridian Bet.
Akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti wa Riadha Mkoa wa Ruvuma, Christian Matembo, alielezea kufurahishwa na muitikio wa washiriki mwaka huu ambao walifikia zaidi ya 200 walijitokeza huku watoto wakitia for a.
Baada yam bio, tamasha linaendelea leo kwa maonyesho ya wajasiriamali, mashindano ya ngoma za asili.

No comments:

Post a Comment

Pages