HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 15, 2019

Kombe la SportPesa Mubashara ndani ya DStv


·        SuperSport yapata idhini kuonyesha mechi zote za michuano hiyo
·        Wababe wa Soka Afrika Mashariki kutunishiana misuli
·        Mshindi kupata fursa ya kucheza na Everton FC

Dar es Salaam, Tanzania - Jumanne, 15 Januari 2018 --- Wapenzi wa kandanda Afrika Mashariki, wanauanza mwaka huu kwa burudani ya aina yake kwa kushuhudia mubashara michuona maarufu ya Kombe la SportPesa itakayoonyeshwa ndani ya DStv kupitia SuperSport ambayo imepata idhini ya kuonyesha michuano hiyo kama mshirika rasmi.

Michuano hiyo itakayofanyika jijini Dar es Salaam itahusisha vigogo 8 wa soka kutoka Tanzania na Kenya na itatimua vumbi kuanzia Januari 22 hadi 27. Michuano hiyo itakuwa na mvuto wa aina yake hasa ukizingatia ukubwa na umaarufu wa timu zinazoshiriki zikiwemo watani wa jadi Simba na yanga, Mbao FC pamoja na Singida United kutoka Tanzania na vigogo wa soka Gor Mahia, AFC Leopard, Bandari FC and Kariobangi Sharks kutoka Kenya

Michuano hiyo itakuwa na mvuto wa aina yake kwani mbali na ukubwa, umaarufu na utani wa timu shiriki, pia kila timu itataka kutwaa kombe hili na hatimaye kupata fursa ya kucheza na moja ya timu maarufu ya soka nchini Uingereza – Everton FC

No comments:

Post a Comment

Pages