HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 22, 2019

ULEGA AAGIZA AFISA MIFUGO KATIKA MANISPAA YA TABORA AUCHUNGUZWE

NA TIGANYA VINCENT

NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega ameagiza Afisa Mifugo wa Manispaa ya Tabora Cornelius Masawe achunguzwe na achukuliwe hatua baada ya kutuhimiwa na wafanyabiashara wa mifugo wa Mnada wa Ipuli kuwanyanyasa ikiwemo kuwatoza malipo zaidi bila kuwapa stakabadhi.

Alisema tuhuma hizo ni nzito kwa kuwa zinaweza kusababisha Serikali kukosa mapato yake ikiwa wafanyabaishara hao watakaa kupeleka mifugo mnadani.
Ulega alitoa kauli hiyo jana wakati wa mkutano na wafanyabiashara wa mifugo kuhusu kuondoa mvutano ulikouwa umezuka katika Mnada wa Ipuli uliopo Manispaa ya Tabora kuhusu utaratibu wa usafirishaji ng’ombe kutoka na kuingia.

Alisema kuwa ni vema vyombo vinavyohusika ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) na vyombo vingine kuchunguza tuhuma zilizotolewa na wafanyabiashara hao wa mifugo dhidi ya Masawe za kutoza fedha za faini ya mifugo bila ya kukatia stakanadhi au kutoa ambayo halingani na malipo yaliyotolewa.

Kufuatia tuhuma hizo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri aliagiza Masawe akamatwe na Polisi kwa ajili ya mahojiano na TAKUKURU , kwa kushirikiana na Polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya kiusalama.

Alisema wafugaji kama makundi mengine Mkoani Tabora wana haki sawa na haipaswi kunyanyaswa na ikitokea wamenyanyaswa ni vema wakatoa taarifa mapema ili hatua ziweze kuchukuliwa.

Mwanri alisema tuhuma zilizotolewa na wafanyabiashara hao ni nzito haiwezekani zikapuuziwa ni vema hatua zikachukuliwa ili kubaini ukweli na ikibidi na hatua za kulifilisha katika maamuzi zifanyike haraka.

Baadhi ya wafanyabishara walisema Masawe wakati wa kuendesha operesheni amekuwa akiwakata na kuwapiga watu wanaokutwa na ng’ombe katika maeneo ambayo hayakatazwi kisheria.

Walisema ameweka migambo katika kila pande ya kuelekea Mnadani ili kuwavizia na anawakamata anawatoza shilingi 50,000/- kila ng’ombe kwa madai kuwa wanapita njia zisizo rasmi.

Walisema Masawe alishawi kupokea shilingi 900,000/- lakini aliandika stakabadhi ya laki 5 tu.
Walisema amekuwa akiendesha zoezi hilo wakati akijua njia za kupitishia mifugo kwenda Mnadani zimevamiwa na watu mbalimbali na kujenga.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo amsema kuwa utaratibu wa nyuma wa kupeleka mifugo katika Mnada wa Ipuli uendelee kutumika wakati suluhusho la kudumu kuhusu kuendelea au kuhamisha likifanyiwa kazi kutokana na eneo hilo kuwa katikati ya mji hivi sasa likitafutwa na pande zote.

Aliwataka wafugaji kuendelea kutii Sheria zilizopo za Manispaa wakati wanaendelea kulitafutia ufumbuzi wa kudumu suala lao la kupitisha ng’ombe kutoka kwao kwenda mnadani.

Ulega alisema tatizo kubwa lilisababisha mvutano huo ni makosa yaliyofanyika nyuma ya kushindwa kulinda njia ya kusafirisha ng’ombe kutoka maeneo mbalimbali na kwenda katika Mnada wa Ipulu na kusababisha watu kujenga.

No comments:

Post a Comment

Pages