HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 28, 2019

enMet YAWEKA MALENGO MATATU YA ELIMU


Na Danson Kaijage, Handeni

CLEMENT  Maganga mbaye ni Mwakilishi wa Mratibu wa Mtandao wa Elimu Tanzania Ten/Met amesema kuwa mtandao wa elimu nchini imejiwekea malengo makuu matatu ya kuimarisha elimu.

Akizungumza na wananchi,wadau wa elimu pamoja na wanafunzi wakati wa Uzinduzi wa Maadhimisho Wiki ya Elimu iliyofanyika kitaifa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga leo amesema kuwa malengo hayo matatuni ni pamona na kuongeza uelewa kwa Umma juu ya haki elimu iliyo bora.

Alitaja malengo mengine kuwa ni kuhamasisha serikali kuzingatia makundi yaliyokosa fursa kama wenye ulemavu,wito wa upatikanaji wa miundombinu na vifaa vya shule,mafunzo ya walimu ikiwa ni pamoja na walimu wenye ulemavu.

Ameyataja malengo mengine kuwa ni pamoja na kuhamasisha na kukumbusha jamii,Serikali na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kuhusu umuhimu wa uwajibikaji wa pamoja katika masuala ya Elimu na utekelezaji wa malengo endelevi la nne na la Tano.

"Mkoa wa Tanga hasa Wilaya ya Handeni kumechaguliwa kuwa sehemu ya kufanyia maadhimisho kutokana na juhudi zanazofanywa na wilaya hasa katika upande wa Elimu jumuishi"alieleza Clement.

Kwa upande wa baadhi wanafunzi wa kike walisema kuwa wanakabiliana na changamoto mbalimbali ya kukatisha masomo ikiwa ni pamoja na miundombinu kutokuwa rafiki.

Wakizungumza na waandishi wa habari wanafunzi hao wa kike walisema umbali wa kati ya shule na nyumbani unachangia zaidi wanafunzi wa kike kurubuniwa na waendesha pikipiki maarufu mama Bodaboda.

Hadija Omari ambaye ni mwanafunzi wa kike alisema changamoto nyingine ambayo wanafunzi wanatukana nayo ni pamoja na ukata unaotokana na familia zao kwa familia kushindwa kuwapatia mahitaji wanayoyataka.

Naye mkuu wa Mkoa wa Tanga Martin Shigera wakati akizindua maadhimisho ya wiki ya Elimu Kitaifa wilayani Handeni alisema kuwa serikali inatambua umuhimu wa asasi zisizokuwa za kiserikali zinavyokuza na kuhamasisha umuhimu wa elimu na ubora wa Elimu nchini.

Shigera alisema kuwa pamoja na mambo mengine mkoa umejiwekea marengo ya kuifanya elimu kuwa shirikishi kwa jamii ili kuhamikisha inapandisha kiwango cha ufaulu.

No comments:

Post a Comment

Pages