HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

September 04, 2019

DENI LA MILIONI SABA KUWAPELEKA MAHAKAMANI

 Na Lydia Lugakila 

Wazazi na walezi wa wahitimu wa wanafunzi wa darasa la saba mwaka huu katika Shule ya Msingi Jamia English Medium Nursery And  primary school iliyopo Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wametakiwa kumaliza  deni la Sh. Milioni Saba wanalodaiwa kutokana na ununuzi wa gari la shule kabla ya kupelekwa mahakamani.

Kauli hiyo imetolewa leo  Septemba 4, 2019 na mwenyekiti wa bodi ya shule ambaye pia ni Sheikh wa Mkoa wa Kagera Sheikh Haruna Kichwabuta katika mahafali ya shule ya msingi Jamia  English Medium Nursery And  primary school wakati akielezea maendeleo ya shule hiyo.

Sheikh Kichwabuta amesema baadhi ya  wazazi na walezi wa wanafunzi wa shule hiyo wamekuwa wakipigiwa simu mara kwa mara na wengine kuandikiwa barua zinazowahimiza kukamilisha deni hilo ambapo wazazi hao wamekuwa wakahidi.

Akielezea Deni linaloikabili shule hiyo amesema lengo na madhumuni ya kuletwa kwa gari hilo shuleni hapo ilikuwa ni kuwasaidia watoto wanaoenda shule na kurudi nyumbani baada ya masomo kutokana na wanafuzi hao kupata adha kubwa ikiwemo jua kali umbali mrefu na Mvua.

Amesema kuwa jambo la kushangaza gari hilo licha ya kuwepo shuleni hapo wazazi hawalitumii ambapo wanadai kuwa watoto wao watatembela miguu ambapo wengine utoka mbali na kusababisha kuchelewa kufika shuleni hapo.

Kutokana na deni hilo mwenyekiti huyo amesema kuwa uwezekano wa kuwafikisha wazazi hao mahakamani ni mkubwa sana huku akiwataka baadhi ya wazazi wengine kumalizia ada za watoto wao wanaohitimu Elimu ya msingi ili kusaidia wanafunzi wanabakia shuleni hapo kusoma kwa amani.

 ‘’Mimi  siwezi kupigwa presha bure Hawa wanafunzi wanamaliza  mwaka mzima  mtoto analipa laki moja zimeandikwa barua ya kuwataka mara kwa mara kulipa michango hiyo lakini wazazi hamkutii tuwapeleka mahakamani wazazi walioshindwa kulipa michango ya shule ikiwemo deni la gari la shule’’amesema.

kwa upande wao baadhi ya wazazi wa wahitimu hao ambao hwakupenda majina yao yatajwe wameiomba shule hiyo kuwasamehe ili waanze kulipa kidogo kidogo.

kwa upande wake Mwalimu mkuu wa shule hiyo Bi Nuriat Nuru amesema kuwa shule hiyo imekuwa ikifanya vizuri kitaaluma licha ya changamoto mbali mbali ikiwemo  ulipaji mbaya wa ada ya shule kwa wazazi, chumba maalumu kwa ajili ya watoto wa kike.

Wahitimu hao wametoa pongezi kwa uongozi wa shule hiyo kwa kuwapatia elimu nzuri yenye maadili na kuwaomba wazazi wao kuona umuhimu wa kuchangia maendeleo ya shule.

Wametoa pongezi kwa mwalimu wa taaluma na  mfundishaji wa somo la kiingereza Shakiru Kalembalemba  kwa  kuwatoa mbali na kuwaivisha katika lugha hiyo.

Akijibu suala hilo la deni la shilingi milioni 7 la gari hilo mgeni rasmi katika mahafali hayo Mhandisi Nasir Chakindo amechangia shilingi laki 3 na kuungwa mkono na wadau mbali mbali waliochangia shilingi laki 7 huku akiwataka wazazi hao kuchangia maendeleo ya shule ili kutowavunja moyo walimu.

No comments:

Post a Comment

Pages