Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James (katikati) ,
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salam katika
uzinduzi wa Mfumo wa Kielekroniki wa Utoaji Leseni za Udalali na
Waendeshaji minada. (Na Mpiga Picha Wetu).
Na Faraja Ezra
KATIBU
Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James amezindua Mfumo wa
Kielekroniki wa utoaji leseni za udalali na uendeshaji wa minada ambao
utasaidia kurahisisha upatikanaji wa huduma hizo.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Katibu huo alieleza
kuwa Mfumo huo utaongeza ufanisi na tija katika kutekeleza majukumu ya
kiserikali ya uendeshaji wa minada na utoaji wa leseni.
Pia
alisema Wizara imekuwa ukifanya jitihada kubwa katika ili kuboresha
huduma hiyo, na kwamba kwa sasa huduma hiyo hupatikana kwa njia ya
compyuta na simu ya kiganjani.
"
Hakuna haja ya kupoteza muda kwa kusafiri wizarani kusajiliwa hivi sasa
Wizara ya Fedha umeona kuwa hiyo ni changamoto hivyo, imeanzisha Mfumo
huo wa Kielekroniki ili kuwarahisishia huduma wananchi wake" alisema
Doto.
Aidha pia kutokana
na ukuaji wa Sayansi na teknolojia hivi sasa Wizara imeona kuna
umuhimu wa kuwa na mfumo huo ili kuondoa usumbufu kwa kufuatilia utoaji
wa leseni ili kuendana na ulimwengu wa kisasa.
Pia
kumekuwa na changamoto za waendesha minada na udalali kufanya kazi
kinyume na sheria na wakati mwingine wanawarubuni watu jambo
linaikosesha serikali kipato hivyo Mfumo huo utasaidia kupunguza
madalali feki.
Amewataka
madali kuzingatia sheria iliyowekwa na Mamlaka husika na iwapo yeyote
atakayepatikana akikiuka taratibu hizo anayeenda kwa kweli hatuna
huruma nao. hatutasita kumchukulia hatua Kali za kinidhamu.
"Maana
siku hizi wapo madalali feki wanaodanganya wananchi kuwa wana vibali
halali vya kutoa leseni na wakati mwingine kuwarubuni ili kukidhi
mahitaji yao sasa kupitia Mfumo huu tutawafahamu madalali feki" alisema.
Alisema mfumo pia utawezesha kupata uhalali wa leseni kwa haraka na uwazi kwa kukomesha ufisadi na utarahisisha kazi.
Amewataka
madalali kusajiliwa katika mfumo huo kwa Mujibu wa sheria na kwamba
kwa yeyote atakayekiuka sheria hiyo atachukuliwa hatua stakiki.
Doto alisema kuanzia leo maombi yote ya usajili yaataanza kupitia simu ya kiganjani na kompyuta.
No comments:
Post a Comment