HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 28, 2020

RC TABORA ASEMA HALMASHAURI ISIYOTENGA SHILINGI 1,000 KWA KILA MTOTO CHINI YA MIAKA MITANO BAJETI YAKE HAITAPITA

  Afisa Lishe Mkoa wa Tabora Monica Yesaya akitoa maelezo mafupi jana kuhusu mambo muhimu yanayohitaji katika masuala ya lishe wakati  kikao cha tathimini ya nusu mwaka ya mkataba wa lishe kwa ngazi ya Mkoa. 

NA TIGANYA VINCENT

MKUU wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amesema hatapitisha bajeti ya Halmashauri itakayoshindwa kutenga shilingi 1,000/- kwa ajili ya kila mtoto aliye chini ya miaka mitano kama ilivyoagizwa.

Alisema kila Halmashauri inatakiwa kupitia mapato yake ya ndani itenge kiasi hicho cha fedha kila mwaka kulingana na idadi ya watoto waliopo katika eneo lao.

Mwanri alitoa kauli hiyo jana wakati akifungua  kikao cha tathimini ya nusu mwaka ya mkataba wa lishe kwa ngazi ya Mkoa.

Alisema katika bajeti ya mwaka ujao wa fedha ni vema kila Halmashauri ihakikishe imetenga fedha hizo ili kukidhi matakwa ya mapambano dhidi ya utapiamlo.

Mwanri alisisitiza kuwa Halmashauri ambayo haitaweka wazi mipango yake haitapita wakati wa Kikao cha Ushauri cha Mkoa (RCC) cha kupitia bajeti.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alisema masuala ya lishe lazima yawe ajenda ya kudumu ya kuanzia ngazi za vijiji hadi Mkoa na kwenye nyumba za Ibada.

Naye Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu alisema asilimia 25.8 ya watoto mkoani humo wamedumaa  na hawana uwezo wa kufundishika na kuleta tija katika uchumi wa Taifa.

Aliwataka Maafisa wanahusika na mipango na bajeti kuhakikusha wanashirikiana na Makatibu wa Afya na Maafisa Lishe kupanga mipango lishe kwenye bajeti.

No comments:

Post a Comment

Pages