HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 26, 2020

SERIKALI YAPONGWEZA KUHAMISHA SIMBA 17

NA GOODLUCK HONGO
MHADHIRI  wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dk.Elikana Kalumanga amesema uamuzi wa serikali wa kuwahamisha wanyamapori aina ya Simba 17 wa familia moja kwenda katika hifadhi mpya ya Buguri-Chato  unapaswa kupongezwa.

Kauli hiyo ilitoa jijini Dar es Salaam juzi na wakati wa mafunzo ya siku mbili kwa waandishi wa habari za mazingira yaliyoandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Mazingira nchini (JET)  kwa kushirikiana na USAID PROTECT.
Mwezi Februari mwaka huu,Serikali kupitia idara ya wanyamapori iliwasafirisha Simba 17 wa familia moja yakiwemo madume mawili kwa ajili ya kuwaweka katika hifadhi mpya ya Chato-Bugiri mkoani Geita.
Akizungumzia suala hilo alisema wanyama wanaishi kulingana na mazingira waliyoyazoea kama walivyo viumbe wengine duniani hivyo kuchukua familia nzima ya Simba hao kutawapa furaha katika makazi yao mapya ambayo itawasaidia kuendelea kuishi hadi watakapozoea mazingira hayo mapya.

Alisema wanyamapori kama Simba,Tembo na wengine huwa na tabia zao hivyo kuwahamisha bila kufuata na kuzingatia mahitaji yao muhimu kunaweza kusababisha waishi wa huzuni na wakati mwingine wanaweza kufa.

Dk.Elikana Kalumanga ambaye ni mtaalamu wa sekta ya wanyamapori kutoka UDSM,alisema Simba huwa na tabia ya kuishi pamoja kama familia ambapo kila baada ya mwaka mmoja Simba dume hupigana na Simba mwenzake dume na atakayeshinda ndiye atayeendelea kuishi na familia.

Alisema ikiwa Simba dume mwenye familia anaweza kuuawa na mwenziwe basi hata watoto nao wanaweza kuuawa wote ili Simba huyo mpya aweze kuwa na familia yake.

“Tunaipongeza Serikali kwa uamuzi wa kuwahamisha Simba wa familia moja kutoka hifadhi ya Serengeti hadi Chato-Bugiri kwa kuwa hata wanyama nao huwa na huzuni wanaipoishi mbali na familia zao na wanaweza kufariki hivyo kuhamishwa kwao kulifuata taratibu za kuwalinda wanyama hao”alisema Dk.Kalumanga

Alisema hata Tembo huishi kwa familia moja miaka yao yote ambapo baadhi ya wanyama pia kama digidigi ambao nao huishi pamoja kama familia lakini ikitokea mmoja kati ya mume au mke akafariki basi aliyebaki ataishi peke yake hadi mwisho wa maisha yake.

“Wanyama waliopo katika hifadhi ya Ruaha,Mikumi na Serengeti wanatofauti kutokana na mazingira wanayoishi ambapo ukamataji wa wanyama unaofanywa na Simba katika Mbuga ya Serengeti ni tofauti na ule wa Simba aliyeko Mikumi au Ruaha kutokana ana uwepo wa misitu”alisema Dk.Kalumanga.

Katika mafunzo hayo,waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari walipata fursa ya kujifunza tabia za wanyamapori,ujangili,masoko ya nyara za wanyamapori,sheria pamoja na utalii.

Mkurgenzi Mtendaji wa JET John Chikomo alisema chama hicho kitaendelea kutoa mafunzo kwa waandishi wa  habari ili waliasaidie taifa katika masuala la uhifadhi wakiwemo wanyamapori.

No comments:

Post a Comment

Pages