HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

April 25, 2020

RC Gambo awaonya Wenyeviti wa Mitaa vijiji na Vitongoji

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo, akipata maelezo kutoka kwa viongozi wa JWTZ wakati walipofika kukagua mipaka ya eneo hilo ikiwa ni kujionea na mwisho kutoa maamuzi ya mgogoro huo.

Sehemu ya makazi ya wananchi wa eneo la Loswira kata ya Moshono ambao mkuu wa mkoa wa Arusha alipita kukagua mipaka yao na JWTZ kikosi Cha 977 KJ kwenye mgogoro uliodumu kwa muda mrefu.





Na Ahmed Mahmoud, Arusha
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesitisha kwa muda kuendelea na shughuli yeyote kwenye eneo la Losirwa kata ya Moshono hadi Serikali itakapotoa maelekezo mengine ambapo amewaonya wenyeviti wa mitaa kuacha kuchukuwa fedha na kutoa vibali vya ununuzi wa ardhi kwenye maeneo yenye migogoro.

Aidha amezitaka halmashauri za wilaya kuacha kutoa vibali vya ujenzi kwa wananchi kwenye maeneo yenye migogoro kwa kuwa inaleta mikanganyiko kwenye jamii na kuleta ugumu wakati wa kuitatua.

Gambo ametoa kauli hiyo wakati alipotembelea eneo lenye mgogoro baina ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi Cha 977 KJ na wakazi wa eneo la Losirwa kata ya Moshono jijini Arusha uliodumu kwa muda mrefu.

Akizungumza baada ya kukagua eneo hilo na kusikiliza pande zote ametoa maagizo hayo na kueleza kuwa wananchi waendelee kuwa watulivu hadi Serikali itakapotoa maelekezo mapya kufuatia mgogoro huo.

Alisema kuwa wananchi wengi wanajielewa kama kuna mtu anaendelea na ujenzi aachie hapo hapo hadi Serikali itakapotoa maelekezo mapya.

"Tunaunda tume ya wataalamu kupitia upya na watatoa mapendekezo baada ya taarifa ndipo tutatoa maamuzi lakini kwa Sasa shughuli zote nimezisitisha"

Alibainisha kuwa wenyeviti na tarafa na vijiji wanaopitishia watu vibali vya kununua ardhi watawachukulia hatua za kisheria kwani wao ndio chanzo cha kuwaingiza wananchi kwenye migogoro.

Kwa upande wao wananchi wa eneo hilo Regina Elias na Poulo Mollel wakizungumza wameitaka Serikali kuangalia suala hilo kwa kina na kufanya tathmini upya kwani wao wameishi muda mrefu eneo hilo na wanategemea maeneo hayo kwa kujipatia riziki zao za kila siku.

Walisema kuwa fedha walizopata kama fidia bado hazilingani na maeneo yao utakuta mtu amelipwa kiasi kidogo na mwingine amelipwa eneo kama hilo kiasi kikubwa kwa eneo lenye ukubwa kama huo na tathmini imekaa muda wa miaka sita ndipo malipo yamekuja kulipwa bila maandishi yeyote hali inayoleta mkanganyiko kisheria.

"Tunaiomba Serikali yetu kwa kuwa sisi tunategemea kilimo na tumeishi muda mrefu 1960 jeshi limenikuta hapa huku jina langu likiwa halipo kwenye orodha ya malipo naambiwa nikae kifamilia kwani kwenye familia kuna malipo ya fidia kwenye eneo langu naomba mkuu wa mkoa tuangalie kwenye suala hilo"alisema Martha John bibi mwenye miaka 86.

No comments:

Post a Comment

Pages