HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 29, 2020

MAKAMU WA RAIS WA ZANZIBAR ATAJA SIFA ZA MGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR

 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Barozi Seif Ali Idd akisalimiana na Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Manispaa ya Shinyanga wakati wa ziara yake katika Manispaa hiyo kuzindua jengo la Katibu wa Umoja wa Vijana CCM Manispaa ya Shinyanga.
 Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Barozi Seif Ali Idd mara baada ya kukata utepe kuzindua  jengo la Katibu wa Umoja wa Vijana CCM Manispaa ya Shinyanga.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack akizungumza na viongozi  wa CCM Mkoa wa Shinyanga wakati ziara ya Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Barozi Seif Ali Idd iliyowakutanisha viongozi wa chama hicho Mkoani Shinyanga.
 
 
Na Mwandishi Wetu, Shinyanga
 
Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar Barozi Seif Ali Idd ametaja sifa za Mgombea anayefaa kuwa Rais wa Zanziba kuwa mtu ambaye ni mwamini mkubwa wa Muungano kwasababu kiongozi wa sifa iyo kamwe hawezi kuleta mgawanyiko miongoni mwa watu wa Tanzania.
Barozi Seif Ali Idd amesema hayo jana alipokutana na viongozi na wanachama wa CCM wa Manispaa ya Shinyanga katika ziara yake kichama mkoani shinyanga inayoendelea baada ya kufanya ziara kama hiyo katika Wilaya ya Kahama.
Barozi Seif aliongeza kuwa kiongozi anayetaka kuwa Rais wa Zanzibar lazima awe yule asiyeweza kutugawa na anayefuata misingi ya Muungano wetu akiongeza kuwa kwasasa kuna watu wengi sana kutoka bara wanaofanya kazi zao Zanzibar na kuna watu wengi sana kutoka Zanzibar wanaofanya kazi zao Tanzania bara.
Kiongozi huyo mkubwa wa Serikali ya Zanzibar amesema mpaka sasa kuna idadi kubwa ya watu ambao tayari wamechukua fomu za kugombea nafasi ya urais wa Zanzibar ambao kimsingi wanatimiza haki yao ya kidemokrasia na mchakato wa kumpata mgombea utajulikana baada ya taratibu kukamilika.
Katika ziara yake Mkoani Shinyanga Barozi Seif Ali Idd alianza na uwekaji jiwe la msingi katika ujenzi wa Nyumba ya Katibu wa Ummoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi na kuwataka vijana wa Chama Cha Mapinduzi kutoshiriki katika vitendo vya rushwa hasa katika kipindi hiki cha uchaguzi.
Aidha amewaonya vijana hao kutokubali kutumiwa kwasababu wagombea wengi upenda kuwatumia vijana kufanikisha malengo yao ya kisiasa na kuwataka kutumia wingi wao kufanikisha uchaguazi hapa Nchini.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Zainab Telack amewataka wagombea nafasi za ubunge Mkoani Shinyanga kutotegemea Msaada wa aina yoyote kutoka Serikalini nakuwataka wagombea hao kujipanga kulingana na matakwa ya chama na kuongeza kuwa serikali itashirikiana nao baada ya kuwa mgombea kuwa amefanikiwa kupita katika mchakato nakufanikiwa kuwa mgombea.
Bi. Telack aliongeza kuwa kutakuwapo na watu wengi watakaojitokeza kuchukua fomu za kugombea ubunge hivyo wagombea wote hao watambue kuwe hawana nafasi yoyote ya kupata msaada kutoka ofisi yake bali wazingatie taratibu zilizowekwa na chama kukidhi matakwa ya taratibu za  uchaguzi. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar yuko Mkoani Shinyanga kwa ziara ya Kichama na ataendelea ziara yake katika Wilaya ya Kishapu na kuendelea kufanya shughuli za Chama kwa kuwa ni mlezi wa Chama hicho Mkoani Shinyanga.

No comments:

Post a Comment

Pages