HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 21, 2020

Mchungaji GCIM aoteshwa upinzani Malawi kushinda uchaguzi mkuu

Mchungaji Yohaness Chawinga wa Kanisa la GCIM Manzese Ubungo jijini Dar es Salaam.




Na Mwandishi Wetu

MUUNGANO wa vyama vya upinzani nchini  Malawi wa Tonse Alliance  chini ya mgombea Urais Dk. Lazarus Chakwera  na  mgombea mwenza  Salous Chilima toka chama cha UTM wametabiriwa kuibuka na ushindi katika uchaguzi mkuu wa marudio unaofanyika kesho.

Utabiri huo umetolewa na Mchungaji Yohaness Chawinga wa Kanisa la Huduma GCIM Manzese Ubungo jijini Dar es Salaam.

Mchungaji Chawinga alisema amekuwa akioteshwa kila mara kuhusu uchaguzi na Bwana Yesu baada ya Mahakama ya Kikatiba nchini humo kuufuta ushindi wa Profesa Athur Mutharika,uliofanyika mwaka Jana.

"Nimekuwa kwenye  maombi  yakuiombea Malawi tangu February  mwaka huu mara nilipopata habari kupitia Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) ya kufutwa kwa matokeo ya uraisi yaliyompa ushindiMutharika.

Toka nilipoanza kuomba na kufunga Mungu amenipa jumbe kuhusu Malawi. Mosi mnamo Machi 15 kupitia ndoto Mungu alinichukua mpaka kazini kwangu nikiwa pale kazini jengo jipya nikamuona  Dk. Lazarus Chakwera baada  ya kukutana naye tukawa tunatembea kwenda  jengo  jipya la  ofisini kwetu huku tukisukuma 'stretcher' na tukiongea lugha ya kimalawi kama  Chitumbuka mara  nikamwambia kwa kiswahili kuwa  utakuwa raisi wa  Malawi," alisema.

'Hii  nikusema kuwa Mungu wa  Mbingu na Nchi amempa kibali  Mch Chakwera kuwa raisi  wa  Malawi. Hivyo huyo ndiye  raisi ajaye wa Malawi.

Njia hii ya ujumbe kama huu wa kukutanishwa na  mgombea wa uraisi kumwambia maneno kama  haya imetokea kwa Rais Donald  Trump na Rais Muhammadu Buhari. Mungu husema nasi kwa njia ya  ndoto, Daniel 7:1 -2  Mwanzo 15:1 Mathayo 1:20,"alisema.

Alisema pili mwezi May alioneshwa amekutana na  mwanamume mmoja  wa Malawi ambapo alikuwa ameshika  nguo  nyekundu akampa yule mwanamume. "Hii naweza kusema kuna kumwagika damu nchini  Malawi. Dalili ya jambo hili imeanza kutokea kwenye kampeni za  mgombea mwenza wa  Mch Chakwera  Mheshimiwa Chilima watu wamejeruhi Kwa risasi na kupigwa mawe," alisema.

Mchungaji Chawinga alisema anawasihi wananchi wa Malawi na jamii ya waaminio kule Malawi  na kwingineko kuombea  uchaguzi uwe wa amani na haki.
 

No comments:

Post a Comment

Pages