HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 27, 2020

Tanzanite za Laizer zitumike kuleta watalii nchini

Anaandika Malisa GJ

Saniniu Laizer mchimbaji mdogo wa madini huko Mererani ameamka Bilionea baada ya kupata mawe mawili ya Tanzanite moja lenye uzito wa 9.2KGs na jingine 5.8KGs yenye thamani ya TZS 7.8 Bilioni.

Watu wengi wanajadili kuhusu Tanzania kumpata Bilionea mpya. Ni jambo zuri lakini kuna jambo jingine ambalo halijadiliwi. Na pengine ni la msingi zaidi kuliko Ubilionea wa Laizer.

Hii Tanzanite ya 9.3KGs inaweza kuwa ndio kubwa zaidi kuwahi kupatikana duniani. Hii ndio "angle"ya habari, ambayo inaweza ikabreak (as breaking news) ikatoa day 2 story na ikatengenezewa developing story hata kwa mwezi mzima.

Kabla ya Laizer kuushangaza ulimwengu kwa kuchimbua ardhi na kupata madini haya makubwa kabisa, Tanzanite kubwa zaidi duniani ilikua na uzito wa 3.3KGs na 16,839 carat. Hii ilichimbwa na kampuni ya TanzaniteOne mwaka 2005.

Kwa mujibu wa mtandao wa www.mining.com Tanzanite hiyo yenye uzito wa 3.3KGs ipo Thailand katika mji wa Bangkok. Wathai wameamua kuifanya fursa ya utalii. Wanatangazia dunia kwamba "karibu Thailand uone Tanzanite kubwa zaidi". Na watu wanasafiri kila pembe ya dunia kwenda kuona hicho kinachoitwa Tanzanite kubwa zaidi na kupiga nayo picha. Utalii wa aina yake.

Kwa kufanya hivyo Thailand iliweza kurudisha fedha ilizotumia kununua Tanzanite hiyo ndani ya miaka minne tu. Na kuanzia 2010 wanapata faida (super normal profit). Mradi huo umeiingizia Thailand pesa nyingi sana na kutoa ajira kwa watu wengi.

Sasa ni wakati wa kibao kugeuka. Na sisi tutengeneze kituo tuweke haya mawe ya Laizer na tuiambie dunia kuwa Tanzanite kubwa zaidi ipo Tanzania na si Thailand tena. Watu waje washangae hayo mawe wapige nayo picha watulipe 'dollars" wakamalizie picknick Serengeti. Wakitaka kumuona na mchimbaji ruksa.

Hii itatulipa zaidi kuliko kuyauza haya mawe kama tulivyofanya 2005. Pia itafungua fursa mpya ya utalii wa madini ambayo hatujawahi kuwa nayo. Tuige kwa Wathai lakini tufanye kwa ubora kuliko wao (ujasusi wa kiuchumi).
_
Kama watu waliweza kusafiri kutoka Marekani, China, UK etc kwenda kushangaa Tanzanite ya 3KGs kule Bangkok, sisi tukisema tunayo ya 9KGs hata shetani si anaweza kuja kushangaa kidogo akapate cha kusimulia kuzimu?

No comments:

Post a Comment

Pages