HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 15, 2020

WAWILI WAJITOKEZA KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS ZANZIBAR

 
Balozi Seif Ali Karume akipokea Fomu kutoka kwa Katibu wa Kamati Maalumu ya NEC Zanzibar na Idara ya Organization.
Kada wa CCM Balozi Ali Karume akionyesha mkoba uliokuwa na fomu ya kugombea Urais wa Zanzibar.


Na Mwandishi Wetu
Makada  wa wawili wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Ali Karume na Mbwana Bakari Juma wamefunguwa dimba la uchukuwaji wa fomu ya kuomba ridhaa kupitia chama hicho kugombea nafasi ya Urais wa Zanzibar.
 Zoezi  hilo la uchukuaji fomu limefanyika katika Ofisi kuu za chama hicho Kisiwandui Mjini Unguja na kukabidhiwa na Katibu wa kamati maalumu ya Zanzibar  na idara Organization Cassin Galos Nyimbo. 
Balozi Ali Abeid Karume ni Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo Zanzibar katika Serikali ya awamu ya Saba ambaye pia ni mtoto wa muasisi Taifa Hili hayati Abeid Karume Rais wa kwanza Visiwani.
 Asubuhi mapema Mbwana Bakari Juma alifika ofisini hapo kabla ya Balozi Ali karume aliyefika saa saba mchana kufanya tendo kama hilo.  
Juma ambaye ni  mhandisi alikiomba chama hicho kumuamini kuwa yeye anaweza kukiwakilisha chama hicho kwenye kuwania nafasi hiyo.
Mara baada ya kuchukua Fomu Balozi Ali Abeid  karume alisema kamba iwapo chama cha Mapinduzi CCM kitampa ridhaa ya kuwa mgombea wa nafasi hiyo na kuwa Rais wa Zanzibar, anatarajia kuendelea dhamira ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuyalinda, kulinda Muungano wa Tanganiyika na Zanzibar na kuendeleza Sera za CCM.
“Iwapo nitateuliwa na chama changu na kupata ridhaa ya wananchi wenzangu, nategemea kuendeleza dhamira ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kwa kuyalinda, kulinda Muungano na kuendeleza Sera za CCM” Alisema Balozi Ali Abeid Karume.

Katika Maelezo yake Balozi Ali Abeid Karume alisema kwamba Dk. Ali Mohamed Shein kwa kushirkiana na Baraza la Mapinduzi amefanya kazi kubwa nay a kupigiw mfano katika kuendeleza Sera zilizoainishwa na Mzee Abeid Amani Karume. 
“Nia yangu ni kuyaendeleza yale yote  mazuri ambayo tumeachiwa na ambayo Jemedari wa Mapinduzi yetu kama vile afya bure,Elimu bure, ugawaji wa Ardhi kwa wananchi na ujenzi wa makazi bora kwa wananchi,”alisema Balozi Ali Abeid Karume. 
Aidha Balozi ali abeid Karume alisema ipo haja ya kuleta usawa wa Kijinisia, kuwalinda watoto, kuwatunza wazee na kuwwapa vijana Elimu ya kujitegemea.
“Pia pindipo nitakuwa mgombea nitakae chaguliwa na chama change na kupewa ridhaa na wananchi wa Zanzibar, Ipo haja ya kuendeleza ujamaa, udugu, upendo na mshikamano ambapo vyete hivyo ndio ngo zetu” alieleza Balozi Ali Karume.
Balozi ali Karume aliwaomba Wananchi wa Zanzibar na Makada wa chama cha Mapinduzi CCM, kumuombea kwa mwenyezimungu katika mchakato huo aliouanza pamoja na kuiombea Nchi na jamii kuwa katika hali ya Amani na utulivu.

Hii ni mara ya Pili kwa Balozi Ali Abeid Karume kuchukua fomu ya kugombania nafasi ya Urais wa Zanzibar ambapo awali alichukua mwaka 2010 ambapo Dk Ali Mohamed Shein ndie alipitishw na Chama cha Mapinduzi kuwa mgombea na kushinda kuwa Rais wa Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Pages