HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

February 07, 2021

TUCTA yaiomba serikali kuwaongezea mshahara wafanyakazi

 

Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA).
 

 

 

NA HAMIDA RAMADHANI, DODOMA


SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Nchini (TUCTA), limeiomba Serikali kuwaongeza mshahara katika bajeti ya Mwaka huu Wafanyakazi katika sekta zote nchini zikiwemo Sekta binafsi kwa lengo la kuwaboreshea maslahi watumishi.

 

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dodoma na Rais wa Shirikisho hilo,Tumaini  Nyamuhoka wakati akifunga Kikao kazi kwa Makatibu wa Chama Cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) yaliliyolenga kuwajengea uwezo.

Nyamuhoka amesema wanampongeza Rais kwa jitihada mbalimbali ambazo amekuwa akizifanya katika kuleta maendeleo huku wakimuomba kuliangalia suala hilo kwa  kina la nyongeza ya mshara yema Sasa 

"Tunampongeza Rais Magufuli kwakuwarudisha kazini watumishi ambao wana Elimu ya darasa la Saba huku akiomba kuwalipa mishara yao kwa kipindi ambacho walikuwa hawapo kazini," amesema Nyamuhoka.

Katika hatua nyingine ametoa wito kwa  Wakurugenzi  Halmashauri,Wakuu wa Taasisi pamoja na Makatibu Tawala Nchini kuacha kuwadharau Viongozi wa Wafanyakazi na badala yake wawape kipaumbele kwa  kuwasikiliza .

Hata hivyo amekemea suala la baadhi ya Maofisa kuwekwa ndani kutokana na kuwapa Fedha Viongozi wao licha ya wao kutokuwa na makosa kutokana na kuagizwa tu kufanya hivyo.

Kwa upande wake Mweka Hazina wa Talgwu Taifa  Siston Mizengo  ameeleza mafanikio yaliyopatikana  kutokana na kuweza kutekeleza mipango yake iliyojiwekea na kwasasa kipo vizuri na ilipata hati Safi.

No comments:

Post a Comment

Pages