HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

May 08, 2021

Benki ya CRDB yakusanya wadau kujadili uvumbuzi katika sekta ya fedha


 

Mkurugenzi wa FSDT, Sosthenes Kewe akiongoza Kongamano lililoandaliwa kwakushirikiana kati ya Benki ya CRDB na Vodacom Tanzania na kuhudhuriwa na maafisa kutoka Wizara ya Elimu, wanafunzi na wakufunzi kutoka vyuo mbalimbali vya Dodoma. Hii ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya wiki ya uvumbuzi “Innovation Week” ambayo yataambatana na Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU).


Meneja Mwandamizi wa Huduma za Ziada za Benki ya CRDB Ndugu Mangire Kibada akizungumza katika kongamano hilo lililofanyika katika viwanja vya Jamhuri Jijini Dodoma.



     Dodoma, Mei 06, 2021 – Benki ya CRDB imefanya kongamano lililobeba mada ya “Ni kwa namna gani sekta ya fedha inapaswa kuenenda kwa mwaka 2021?” ukizingatia dunia inapita katika changamoto ya janga la COVID-19 liloshika kasi mwaka 2020. Kongamano hilo lilioandliwa kwa kushirikiana na kampuni ya simu ya Vodacom liliongozwa na Mkurugenzi wa FSDT, Sosthenes Kewe na kuhudhuriwa na maafisa kutoka Wizara ya Elimu, wanafunzi na wakufunzi kutoka vyuo mbalimbali vya Dodoma.


Kongamano hilo limefanyika ikiwa ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya wiki ya uvumbuzi “Innovation Week” ambayo yataambatana na Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU) yaliasisiwa mwaka 2019 kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI, Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam (DIT), Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA). 


Akizungumza katika kongamano hilo, Meneja Mwandamizi wa Huduma za Ziada za Benki ya CRDB, Mangire Kibada amaesema kuwa Benki ya CRDB imeamua kudhamini wiki ya uvumbuzi kwa kuwa inaamini katika kutoa huduma na bidhaa bora kwa wateja ambazo zinapatikana kwa njia ya kuwekeza katika uvumbuzi.

“Kwetu Benki ya CRDB tunaamini uvumbuzi ni kitu pekee ambacho kinaweza kututofautisha na wengine katika soko na hivyo kuifanya benki yetu kuendelea kuwa kinara sokoni kwa kuweza kutimiza mahitaji ya wateja wa makundi mbalimbali” alisema Kibanda.


Kwa upande wake Mkurugenzi wa FSDT, Sosthenes Kewe alisema kuwa lengo la kongamano hilo ni  kuainisha na kupendekeza hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika kutengeneza na kutekeleza mipango ya uvumbuzi katika sekta ya fedha. 

No comments:

Post a Comment

Pages