HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

December 01, 2021

Utouh azindua Kitabu, awashauri watendaji kutekeleza mapendekezo ya CAG

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu, Ludovick Utouh.
Muonekano wa Kitabu cha LUDOVICK UTOUH.
 
 
Na Hussein Ndubikile, Dar es Salaam

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Mstaafu Ludovick Utouh amezindua Kitabu cha Ukaguzi wa Umma kilichopewa jina Misingi ya Ukaguzi wa Umma (Principle of Public Sector Auditing) na  kuwashauri watendaji wa Serikali kutekeleza mapendekezo yanayotolewa na CAG ili kuboresha usimamizi wa Rasilimali za Taifa.

Kauli hiyo ameitoa jijini Dar es Salaam wakati akizindua kitabu hiicho ambapo amesema kuzinduliwa Kwa Ripoti hiyo kutawasaidia  wananchi kuweza kuelewa namna ya Rasilimali zao zinavyotumika katika kuwaletea maendeleo.

"Ripoti hii inaweza kutumika kama chanzo cha taarifa katika ufuatiliaji wa matumizi na Rasimali za umma kuanzia ngazi ya halmashauri "Alisema Mkaguzi mstaafu utouh.

Amebainisha kuwa kipoti hiyo inafafanua umuhimu wa ukaguzi na maoni ya ukaguzi pamoja na Mambo nane ambayo Serikali inatakiwa kuyafanyiakazi.

Ameyataja mambo hayo ni pamoja na mwendo wa Hati za ukaguzi, mwendo wa utekelezaji wa mapendekezo ya CAG sambamba na maagizo ya kamati ya kudumu ya bunge  ya usimamizi wa Serikali za Mitaa.

Mwandishi wa Kitabu hicho Utouh amesema ameandika kitabu hicho baada ya kubaini kuwapo uelewa mdogo na kukosekana vitabu katika eneo la taaluma yake panapogusa mahususi ukaguzi hesabu za fedha kwenye sekta ya umma.

Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Emmanuel Tutuba amesema kitabu hicho ni silaha muhimu kwa Serikali kupambana na wabadhirifu wa fedha za umma.

Amemwomba Utouh na Taasisi ya Wajibu anayoiongoza kukitafsiri kitabu hicho kwa lugha ya Kiswahili ili kusaidia kila Mtanzania kukisoma na kukielewa kwa wepesi.

Kwa upande wake, Naibu Mkuu wa Ofisi ya CAG, Salina Mkumba amesema kitabu hicho kimezingatia vigezo vyote vya kimataifa katika ukaguzi.

Nae,Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi hiyo, Yona Killagane amebainisha kitabu hicho ni silaha muhimu kwa Maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali na Maofisa wa Ofisi ya CAG.

Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Uongozi, Balozi Ombeni Sefue amewataka viongozi mbalimbali kuwa waadilifu na waaminifu wanapokuwa wakisimamia miradi ya umma.

No comments:

Post a Comment

Pages