HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

January 20, 2022

CCM yampitisha Dk.Tulia kugombea nafasi ya Spika

 


Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapindizi (CCM)Shaka Hamdu Shaka akizungumza na waandishi wa habari.



Na Asha Mwakyonde, Dodoma


KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi(CCM)Taifa imepitisha jina la Naibu Spika wa BungeTulia Ackson kugombea nafasi ya Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Akizungumza leo Jijini Dodoma na Katibu wa Itikadi na uenezi wa Chama hicho Shaka Hamdu Shaka mara baada ya kumalizika kwa kikao maalum ambacho kimeketi leo Chini ya Mwenyekiti wake Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Shaka amesema kwa mujibu wa katiba ya Chama cha Mapinduzi kikao hicho ni kwa mujibu wa taratibu za Katiba ya Chama kilikuwa kinatathmini utendaji wa Serikali zote mbili na  kimejadili mambo mbalimbali ikiwemo majina ya wanaowania nafasi ya Uspika ambapo  kimetua Naibu Spika Tulia Ackson  kuwania nafasi hiyo.

Katibu huyo ameongeza kuwa  Januari 31, mwaka huu wabunge watapiga kura kumpigia Dk. Tulia.

Mbali na hiliKamati hiyo imempongeza Mwenyekiti wa CCM Taifa katika utendaji wake wa kazi kwakuhakikisha wanafunzi wote nchini wameingia kidato cha kwanza kutokana na kukamilika kwa ujenzi wa madarasa.


Pia kamati hiyo kwa mujibu wa Shaka kikimpongeza  Rais wa Serikali ya mapinduzi Zanzibar kutokana na utendaji wake kwa kusimamia uchumi wa buluu.

Mchakato wa uchukuaji fomu za kuwania nafasi ya Spika wa Bunge ulianza rasmi Januari 10 Mwaka 2022 na kumalizika Januari15 Mwaka huu kufuatia aliyekuwa Spika wa Bunge Job Ndugai kujiuzulu nafasi hiyo mnamo Januari 6 Mwaka huu na kuachwa wazi.
 

No comments:

Post a Comment

Pages