HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 10, 2022

DIWANI SINGIDA AONGOZA HARAMBEE KANISA LA WAADIVENTISTA WASABATO, RAIS SAMIA ATAJWA




Diwani wa Kata ya Mwaru Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Iddi Athumani Makangale (katikati) ambaye ni muumini wa dini ya Kiislam akiongoza harambee ya ununuzi wa vyombo vya muziki vya Kanisa la Waadiventista Wasabato la Kijiji cha Kaugeri katika changizo lililofanyika hivi karibuni ambapo zaidi ya Sh. Milioni 1.7 zilipatikana. Kushoto anayechangia katika harambe hiyo ni Afisa Mtendaji wa Kata ya Kaugeri, Ukunde Mshele.
Mchungaji Kiongozi wa kanisa hilo,  Geofrey Mgonja akizungumza wakati akimshukuru Diwani Makangale kwa   kuongoza harambee hiyo. Katikati aliyefunga skafu ni Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tawi la Kaugeri, Hassan Omari.
 

Na Dotto Mwaibale, Singida

 

DIWANI wa Kata ya Mwaru katika Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, Iddi Athumani Makangale ambaye ni muumini wa dini ya Kiislam ameongoza harambee ya ununuzi wa vyombo vya muziki vya Kanisa la Waadiventista Wasabato la Kijiji cha Kaugeri ambapo zaidi ya Sh. Milioni 1.7 zilipatikana.

Akizungumza katika changizo hilo Makangale alisema amejisikia furaha ya kualikwa kuongoza harambee hiyo hasa ikizingatiwa kuwa yeye ni Muislam jambo ambalo limezidi kuongeza mshikamano baina ya Waislam na Wakristo.

" Tukio ili limenipa furaha sana n.a. linaonesha ni jinsi gani waumini wa hizi dini mbili wanavyoshirikiana katika shughuli zao" alisema Makangale.

Alisema katika harambee hiyo iliyoonesha mafanikio makubwa jumla ya Sh. 1,785,000 zilipatikana huku ahadi zikiwa ni Sh.470,000.

Diwani Makangale alitumia nafasi hiyo kuwaomba viongozi wa dini hizo na waumini wao kuendelea kudumisha ushiriano huo katika shughuli mbalimbali jambo litakalosaidia kuharakisha maendeleo katika kata hiyo.

Akizungumza baada ya harambee hiyo  Mchungaji Kiongozi wa Kanisa hilo Geofrey Mgonja alisema wamefarijika sana kwa harambee hiyo iliyoongozwa na diwani huyo na kueleza ni jambo la kuigwa kwa waumini wote wa dini hizo.

Alisema tukio la namna hiyo liliwahi kufanywa na Aliyekuwa Rais wa Tano wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli pale alipoongoza harambee ya ujenzi wa Msikiti wa Chamwino mkoani Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Pages