HABARI MSETO (HEADER)


Breaking

June 05, 2022

Wanawake Mtwara wampa tuzo maalumu Rais Samia

Wanawake mkoani Mtwara, wamemkabidhi tuzo maalumu Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua mchango wa kuwatumikia Watanzania katika kuwaletea maendeleo hususan mkoani humo.

Akizungumza baada ya kupokea tuzo hiyo, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amesema tuzo hiyo itamtia moyo na kumpa ari Rais Samia katika kuwatumikia Watanzania.

"Kitendo cha kumpatia tuzo mnamtia moyo, mnapa ari ya kuwatumikia Watanzania, lakini pia mnamtia ari ya kutimiza malengo yenu akinamama katika mambo muhimu na ya msingi kama ambavyo nimeshasema.

"Wito wangu kwenu msisite, msiishie hapa endeleeni kumuombea kwa Mwenyezi Mungu, kila mmoja kwa imani yake Mwenyezi Mungu azidi kumpa afya njema ili aweze kututumikia Watanzania," amesema.

Akiendelea kuzungumza zaidi kuhusu tuzo hiyo, Shaka amesema aliyoyafanya Rais Samia wanawake wanayajua hata ukiwaamsha usingizini wanakwambia ameifungua Mtwara.

Awali akizungumza kabla ya kukabidhi tuzo hiyo, kwa niaba ya wanawake hao Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania Mkoa wa Mtwara, Zuhura Farid, amesema wanawake wa Mtwara kwa niaba ya wanawake wengine wote wanampongeza Rais Samia kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya.

"Hivyo tunaomba tukukabidhi zawadi hii kwa heshima na taadhima tunaomba umfikishie zawadi hii mama na umwambie asichelewe kufika Mtwara aje atuone kinamamma," amesema.

No comments:

Post a Comment

Pages